-
Jinsi Yehova AnavyotuongozaMnara wa Mlinzi—2000 | Machi 15
-
-
(Mithali 7:24) Jambo hili lawahusu watoto wetu pia. Mtoto anapoenda shuleni, inatarajiwa amsikilize mwalimu, hata kama hapendi somo fulani au kama inaonekana haelewi somo hilo. Mwalimu ajua kwamba mtoto huyo akijaribu kusikiliza, angalau atapata manufaa fulani kutokana na somo hilo. Basi, je, si jambo linalopatana na akili kwa watoto wenye umri wa kwenda shuleni kusikiliza mafundisho kwenye mikutano ya kutaniko badala ya kuachiliwa kulala usingizi mara tu mikutano inapoanza? Ni kweli kwamba baadhi ya kweli zenye thamani katika Maandiko ni “mambo fulani magumu kuelewa.” (2 Petro 3:16) Lakini tusipuuze uwezo wa mtoto kujifunza. Mungu haupuuzi. Katika nyakati za Biblia, aliwaamuru watumishi wake wachanga ‘wasikie na kujifunza na kumcha BWANA, na kuangalia kutenda maneno yote ya torati hii,’ ambayo bila shaka ilikuwa na sehemu zilizokuwa ngumu kwa watoto kuelewa. (Kumbukumbu la Torati 31:12; linganisha Mambo ya Walawi 18:1-30.) Je, Yehova hatarajii watoto wetu wafanye vivyo hivyo leo?
8. Wazazi wengine huchukua hatua zipi ili kuwasaidia watoto wao wawe wasikivu kwenye mikutano?
8 Wazazi Wakristo hutambua kwamba mahitaji fulani ya kiroho ya watoto wao hutoshelezwa na yale wanayojifunza kwenye mikutano. Kwa hiyo, wazazi wengine hupanga watoto wao walale usingizi kwa muda mfupi kabla ya kwenda mikutanoni ili wafike kwenye Jumba la Ufalme wakiwa wamepumzika na tayari kujifunza. Wazazi wengine wanaweza kuzuia kabisa au kuwakataza kwa hekima watoto wao wasitazame televisheni jioni ambayo kuna mkutano. (Waefeso 5:15, 16) Na wazazi kama hao hufanya watoto wasikengeushwe, wakiwatia moyo wasikilize na kujifunza, kulingana na umri wao na uwezo wao.—Mithali 8:32.
-
-
Jinsi Yehova AnavyotuongozaMnara wa Mlinzi—2000 | Machi 15
-
-
10, 11. Wazazi wengine wamewasaidiaje watoto wao wawe wasikivu zaidi, na ni njia zipi ambazo wewe umeona kuwa zenye msaada?
10 Mazoea mazuri ya kusikiliza hukuzwa kwa njia bora wakati wa utoto. Hata kabla hawajajifunza kusoma na kuandika, watoto fulani ambao hawajaanza kwenda shuleni hutiwa moyo na wazazi wao “kuandika” wakati wa mikutano. Wao hutia alama fulani kwenye karatasi wakati maneno ya kawaida kama “Yehova,” “Yesu,” au “Ufalme” yanapotumiwa. Kwa njia hiyo, watoto wanaweza kuwa makini kusikiliza yale yanayosemwa jukwaani.
11 Nyakati nyingine hata watoto wakubwa huhitaji kutiwa moyo wasikilize. Baba mmoja alipotambua kwamba mawazo ya mwana wake mwenye umri wa miaka 11 yalikuwa mbali wakati wa mkusanyiko wa Kikristo, alimpa Biblia na kumwambia afungue maandiko yaliyokuwa yakitajwa na wasemaji. Baba yake, aliyekuwa akiandika mambo makuu, alikuwa akimtazama mwana wake akitumia Biblia hiyo. Basi, mwana huyo akafuata programu ya mkusanyiko kwa shauku zaidi.
-