-
Utatazama Sinema Zipi?Amkeni!—2005 | Mei 8
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 12]
‘SISI HUFANYA MAAMUZI PAMOJA’
“Nilipokuwa mdogo, tulienda kwenye sinema tukiwa familia. Kwa kuwa sasa nina umri mkubwa, ninaruhusiwa kwenda peke yangu. Hata hivyo, kabla ya kuniruhusu kwenda, wazazi wangu hutaka kujua kichwa cha filamu hiyo na habari inayozungumziwa. Ikiwa hawajui jambo lolote kuhusu sinema hiyo, wao husoma maoni ya wachambuzi au kutazama sehemu ndogo ya sinema hiyo inapoonyeshwa kwenye televisheni. Pia wao hutafuta habari kuhusu sinema hiyo kwenye Intaneti. Wakihisi kwamba sinema hiyo haifai, wao hutoa sababu. Vilevile wao huniruhusu nitoe maoni yangu. Sisi hujieleza waziwazi na kufanya maamuzi pamoja.” —Héloïse, mwenye umri wa miaka 19, anayeishi Ufaransa.
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 13]
ZUNGUMZIENI MAMBO HAYO!
“Wazazi wakiwakataza watoto wao vitumbuizo fulani na kukosa kuwapa vitumbuizo vinavyofaa, huenda watoto hao wakajaribu kutosheleza tamaa zao kwa siri. Kwa hiyo, watoto wanapotaka kutazama sinema zisizofaa, wazazi fulani hawawakatazi moja kwa moja, wala kuwaruhusu. Badala yake, wao hungoja hali itulie. Bila kukasirika, wao huzungumzia mambo hayo kwa siku kadhaa, wakimwuliza kijana huyo sababu inayofanya ahisi kwamba sinema hiyo inafaa. Wanapozungumzia jambo hilo, mara nyingi vijana hukubaliana na wazazi wao na hata kuwashukuru. Kisha, wakiongozwa na wazazi wao, wao huchagua vitumbuizo vingine wanavyoweza kufurahia pamoja.”—Masaaki, mwangalizi asafiriye huko Japani.
-
-
Utatazama Sinema Zipi?Amkeni!—2005 | Mei 8
-
-
Manufaa ya Dhamiri Iliyozoezwa
Biblia huzungumza kuhusu wale ambao “nguvu zao za ufahamu zimezoezwa kutofautisha yaliyo sawa na yaliyo makosa pia.” (Waebrania 5:14) Kwa hiyo, lengo la wazazi linapaswa kuwa kukazia viwango ambavyo vitawasaidia watoto wao kufanya maamuzi yenye hekima watakapokuwa na uhuru wa kuchagua vitumbuizo vyao.
Kuhusiana na jambo hilo, vijana wengi ambao ni Mashahidi wa Yehova wamezoezwa vizuri na wazazi wao. Kwa mfano, Bill na Cherie, wanaoishi Marekani hufurahia kwenda kutazama sinema pamoja na wavulana wao wawili. Bill anasema, “baada ya kutazama sinema hiyo, mara nyingi sisi huzungumza kuhusu filamu hiyo, ilifundisha maadili gani na ikiwa tunakubaliana na maadili hayo au la.” Bila shaka, Bill na Cherie wanatambua umuhimu wa kuwa wateuzi. Bill anasema, “Sisi hufanya uchunguzi kuhusu filamu hiyo kabla ya kuitazama, na hatuoni aibu kutoka kwenye jumba la sinema ikiwa kuna jambo lisilofaa ambalo hatukuwa tumetarajia.” Kwa kuwahusisha watoto wao kufanya maamuzi mazito, Bill na Cherie wanahisi kwamba wanawasaidia wana wao kusitawisha mtazamo unaofaa kuhusu mema na mabaya. Bill anasema, “wanafanya maamuzi ya hekima zaidi wanapochagua filamu watakazotazama.”
Kama Bill na Cherie, wazazi wengi wamewasaidia watoto wao kuzoeza nguvu zao za ufahamu kuhusiana na vitumbuizo. Ni kweli kwamba sinema nyingi ambazo watayarishaji wa filamu hutokeza hazifai. Kwa upande mwingine, wanapoongozwa na kanuni za Biblia, Wakristo wanaweza kufurahia vitumbuizo vinavyofaa na kuburudisha.
-