Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sehemu ya 2—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Kutoka Brazili, Ndugu Young alisonga mbele hadi Argentina katika 1924 na kupanga ugawanyaji wa bila malipo wa fasihi 300,000 katika Kihispania katika 25 kati ya ile miji na majiji makubwa. Mwaka huohuo yeye binafsi alisafiri pia kwenda Chile, Peru, na Bolivia ili kugawanya trakti.

  • Sehemu ya 2—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Wakati huohuo, alipowasili katika Argentina, Ndugu Muñiz alikuwa ameanza kuhubiri upesi, huku akijiruzuku kwa kurekebisha saa. Kuongezea kazi yake katika Argentina, alitoa uangalifu kwa Chile, Paraguai, na Uruguai. Kwa ombi lake baadhi ya ndugu walitoka Ulaya ili kutoa ushahidi kwa idadi ya watu wasemao Kijerumani.

  • Sehemu ya 2—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Mwingine aliyekuwa na roho ya painia halisi alikuwa Richard Traub, aliyekuwa amejifunza kweli katika Buenos Aires. Alikuwa na hamu ya kushiriki habari njema pamoja na watu kwenye ile ng’ambo nyingine ya Andes, katika Chile. Katika 1930, miaka mitano baada ya kubatizwa, aliwasili katika Chile—Shahidi pekee katika nchi ya watu 4,000,000. Mwanzoni, alikuwa na Biblia tu ya kutumia kufanya kazi, lakini alianza kutembelea watu nyumba hadi nyumba. Hakukuwa na mikutano ya kutaniko ambayo angeweza kuhudhuria, hivyo, Jumapili, katika ule wakati wa kawaida wa mikutano, alikuwa akitembea kwenda kwenye Mlima San Cristóbal, na kuketi chini ya kivuli cha mti na kujizamisha katika funzo la kibinafsi na sala. Baada ya kukodi nyumba, alianza kualika watu kwenye mkutano humo. Yule mtu pekee aliyekuja kwa ajili ya mkutano wa kwanza alikuwa Juan Flores, aliyeuliza hivi: “Na wale wengine, watakuja lini?” Ndugu Traub alijibu tu: “Watakuja.” Nao walikuja. Katika muda uliopungua mwaka mmoja, 13 wakawa watumishi wa Yehova waliobatizwa.

      Miaka minne baadaye, Mashahidi wawili ambao hawakuwa wamekutana tena waliungana ili kuhubiri habari njema katika Kolombia. Baada ya mwaka wenye matokeo huko, Hilma Sjoberg alilazimika kurudi Marekani. Lakini Kathe Palm aliabiri kwa meli hadi Chile, akitumia zile siku 17 baharini kutolea ushahidi wafanyakazi na abiria pia. Wakati wa mwongo uliofuata, alifanya kazi kutoka bandari ya Arica ya juu kaskazini, hadi chini kusini, katika Tierra del Fuego. Alizuru sehemu za biashara na akatolea ushahidi maofisa wa serikali. Alifikia kambi za wachimba migodi na malisho ya kondoo ya mbali sana, huku akichukua fasihi zake kwa mfuko alioweka mabegani, alimotia ndani mahitaji yake kama vile blanketi ya kulalia. Hayo yalikuwa maisha ya painia halisi. Na kulikuwa wengine waliokuwa na roho hiyohiyo—wengine wakiwa waseja, wengine wakiwa wamefunga ndoa, vijana kwa wazee.

      Wakati wa mwaka 1932, jitihada ya pekee ilifanywa kueneza ujumbe wa Ufalme katika nchi za Amerika ya Latini ambako kazi kidogo sana ya kuhubiri ilikuwa imefanywa. Katika mwaka huo kile kijitabu The Kingdom, the Hope of the World kiligawanywa kwa njia yenye kutokeza sana. Kijitabu hicho kilikuwa na hotuba iliyokuwa tayari imesikiwa katika matangazo ya redio ya kimataifa. Sasa nakala zipatazo 40,000 za hotuba hiyo kwa namna ya chapa ziligawanywa katika Chile,

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki