Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Biblia Ilivyotufikia—Sehemu ya Tatu
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Oktoba 15
    • BURMA, 1824—Maofisa wa mfalme wametoka tu kupekua makao ya mishonari ya Adoniram na Ann Judson, wakichukua kila kitu walichofikiri kuwa chenye thamani. Lakini wamekosa hazina yenye thamani zaidi—hati ya Biblia iliyotafsiriwa ambayo Ann alikuwa ameficha kisiri chini ya hiyo nyumba. Adoniram, mtafsiri, alala akiwa amefungwa kwa minyororo katika gereza lenye mbu wengi, akishtakiwa kupeleleza. Sasa unyevuanga watisha kuharibu hiyo hati. Yaweza kuokolewaje? Ann aishona ndani ya mto mgumu na kuupeleka kwa mume wake gerezani. Mto huo unahifadhiwa, na yaliyomo yawa sehemu ya Biblia ya kwanza ya Kiburma.

  • Jinsi Biblia Ilivyotufikia—Sehemu ya Tatu
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Oktoba 15
    • Wamishonari na Sosaiti za Biblia

      Katika nchi nyingi, miaka ya 1600 na ya 1700 ilitiwa alama na ongezeko kubwa la usomaji wa Biblia. Uingereza hasa iliathiriwa sana na Biblia wakati wa kipindi hicho. Kwa hakika, hadithi na mafundisho ya Biblia yalipenya mawazo ya karibu kila mtu katika hiyo nchi, toka mfalme hadi kijana mwongoza plau. Lakini uvutano wa Biblia ulienea mbali zaidi. Wakati huo Uingereza ilikuwa serikali yenye kufanya biashara baharini na ya kikoloni, na Waingereza fulani waliichukua Biblia katika safari zao. Hilo liliweka msingi wa kampeni ya Biblia iliyoenea.

      Kuelekea mwisho wa miaka ya 1700, Biblia iliwachochea watu fulani Uingereza kufikiria mahitaji ya kiroho ya wenyeji wa nchi zilizotapakaa za Milki ya Uingereza. Hata hivyo, hangaiko hilo halikuwa la ulimwenguni pote kamwe. Watu wengi wa kanisa waliamini juu ya kuamuliwa kimbele yatakayompata mtu, na kwa hiyo waliyafikiria kuwa mapenzi ya Mungu kwamba watu fulani wasiokolewe. William Carey aliyetarajiwa kuwa mishonari alipotoa hotuba yenye idili ili kuchochea tegemezo kwa ajili ya kutuma misheni India, mtu fulani alipaaza sauti akimkemea: “Keti chini, mwanamume kijana; Mungu atakapo kugeuza makafiri, Atafanya hivyo bila msaada wako!” Hata hivyo, Carey alisafiri kupitia baharini kuelekea India mwaka wa 1793. Kwa kushangaza, hatimaye alitafsiri Biblia nzima au visehemu vyake katika lugha 35 za Kihindi.

      Wamishonari waling’amua kwamba chombo chao cha msingi kabisa kilikuwa Biblia katika lugha ya kienyeji.

  • Jinsi Biblia Ilivyotufikia—Sehemu ya Tatu
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Oktoba 15
    • Sehemu kubwa ya Biblia ni masimulizi na vielezi vitegemeavyo mambo yanayoonwa kila siku. Hilo hufanya iwe rahisi kutafsiri kuliko ikiwa ingeandikwa kwa kutumia mitajo dhahania ya falsafa. Hata hivyo, kama iwezavyo kutabiriwa, jitihada za mapema za wamishonari zilitokeza tafsiri zenye kutatanisha au zenye kuchekesha. Kwa kielelezo, tafsiri moja iliwapa watu katika sehemu fulani ya India wazo la kwamba Mungu ana rangi ya kibluu. Neno lililotumiwa kumaanisha “-a kimbingu” katika usemi “Baba wa kimbingu” lilimaanisha “kuwa na rangi ya anga”—mbingu halisi!

      Kwa habari ya vizuizi vya mtafsiri, Adoniram Judson aliandika hivi mwaka wa 1819: Tunapojifunza lugha inayosemwa na watu sehemu ile nyingine ya dunia, ambao njia zao za kufikiri ni tofauti kabisa na zetu, na ambao kwa hiyo hatufahamu misemo yao, na herufi na maneno hayafanani hata kidogo na yale ya lugha yoyote ile ambayo tumeona; wakati ambapo hatuna kamusi wala mkalimani na ni lazima tuielewe lugha hiyo kidogo kabla hatujaweza kujipatia msaada wa mwalimu wa mahali hapo—hilo lamaanisha kazi!’ Nayo kazi ya watafsiri kama vile Judson iliongeza sana kupatikana kwa Biblia.—Ona chati kwenye ukurasa wa 12.

      Ann Judson alimsaidia mumewe katika ile kazi ngumu ya kutafsiri. Lakini akina Judson walikabili zaidi ya majaribu ya kitaaluma. Maofisa wa mfalme walipomkokota Adoniram hadi jela, Ann alikuwa akitarajia kupata mtoto mchanga. Kwa muda wa miezi 21, akiwa na moyo mkuu, aliwaomba kwa bidii maofisa wenye uhasama wamwachilie mumewe. Masaibu hayo pamoja na ugonjwa ulidhuru afya yake. Muda mfupi baada ya Adoniram kuachiliwa, Ann wake mwenye ujasiri na binti yao mchanga walikufa kutokana na homa. Adoniram alivunjika moyo. Hata hivyo, alimtegemea Mungu ili kupata nguvu naye akaendelea kutafsiri, akikamilisha Biblia ya Kiburma mwaka wa 1835. Wakati huohuo, ubishi mwingine wenye hila juu ya Biblia ulikuwa ukikua.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki