-
Faida za Kujitiisha Katika Mpango wa KitheokrasiTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
Mungu.” (Mt. 22:21) Pia, mipango ya kuhubiri eneo kikamili hupatana na sheria za kulinda taarifa zinazotumiwa. Tukijitiisha na kuheshimu mamlaka halali katika mambo yote ambayo hayapingani na sheria ya Yehova ya uadilifu, tutatumia vizuri nguvu zetu zote katika kazi ya kuhubiri.—Marko 13:10; Mdo. 5:29.
12 Ujitiisho wa kitheokrasi hugusa kila sehemu ya maisha. Kwa macho ya imani, tunatazamia kuiona siku ambayo wanadamu wote watajitiisha kwa Yehova Mungu. (1 Kor. 15:27, 28) Wale wanaokubali kwa shangwe enzi kuu ya Yehova watabarikiwa sana wanapoendelea kujitiisha kwake kwa umilele wote!
-
-
Undugu Wenye UmojaTengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
-
-
SURA YA 16
Undugu Wenye Umoja
YEHOVA MUNGU alishughulika na Waisraeli kwa miaka 1,500 hivi wakiwa taifa lake. Baadaye, Yehova ‘alielekeza uangalifu wake kwa mataifa ili achukue kutoka kwao watu kwa ajili ya jina lake.’ (Mdo. 15:14) Watu kwa ajili ya jina la Yehova wangekuwa mashahidi wake, nao wangefikiri na kutenda kwa umoja popote walipo duniani. Kazi ambayo Yesu aliwapa wafuasi wake ingetokeza kukusanywa kwa watu kwa ajili ya jina la Mungu. Aliwaagiza hivi: “Basi, nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, mkiwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, na kuwafundisha kushika mambo yote niliyowaamuru.”—Mt. 28:19, 20.
Wewe ni sehemu ya undugu wa ulimwenguni pote wa Wakristo wenye umoja ambao hawatenganishwi na tofauti za kitaifa, kikabila, au kiuchumi
2 Umekuwa mwanafunzi wa Yesu Kristo kwa kujiweka wakfu kwa Yehova na kubatizwa. Wewe ni sehemu ya undugu wa ulimwenguni pote wa Wakristo wenye umoja ambao hawatenganishwi na tofauti za kitaifa, kikabila, au kiuchumi. (Zab. 133:1) Kwa sababu hiyo, unawapenda na kuwaheshimu ndugu zako Wakristo kutanikoni. Huenda zamani usingeweza kushirikiana na baadhi yao kwa sababu ya tofauti za kijamii, kitaifa, au kielimu. Mmeunganishwa kwa upendo wa kindugu ulio imara na wenye nguvu kuliko uhusiano mwingine wowote wa kijamii, wa kidini, au wa familia.—Marko 10:29, 30; Kol. 3:14; 1 Pet. 1:22.
-