Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wakumbukeni Wale Wanaoongoza Kati Yenu”
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • yanayofanywa kwa niaba ya watu wa Mungu hutegemea sifa hii bora ya upendo. Kuhusiana na upendo, andiko la 1 Wakorintho 13:4-8 linasema: “Upendo ni wenye subira na fadhili. Upendo hauna wivu, haujigambi, haujivuni, haujiendeshi bila adabu, hautafuti faida zake wenyewe, hauchokozeki. Hauweki hesabu ya ubaya. Haushangilii ukosefu wa uadilifu, bali hushangilia pamoja na kweli. Huhimili mambo yote, huamini mambo yote, hutumaini mambo yote, huvumilia mambo yote. Upendo haushindwi kamwe.” Kwa kuwa upendo ndio msingi wa maamuzi yote yanayofanywa ili kuwanufaisha watumishi wa Yehova, tuna hakika kwamba tutalindwa ikiwa tutatii mwongozo huo. Isitoshe, mwongozo huo ni uthibitisho wa upendo wa Yehova.

      11 Kama ilivyokuwa katika karne ya kwanza, Yehova anatumia wanaume wasio wakamilifu kuwaongoza watu wake. Hata zamani Yehova alitumia wanadamu wasio wakamilifu kutimiza mapenzi yake. Noa alijenga safina na kuhubiri kuhusu uharibifu uliokuwa ukikaribia siku hizo. (Mwa. 6:13, 14, 22; 2 Pet. 2:5) Musa aliteuliwa kuwaongoza watu wa Mungu kutoka Misri. (Kut. 3:10) Wanaume wasio wakamilifu waliongozwa na roho takatifu kuandika Biblia. (2 Tim. 3:16; 2 Pet. 1:21) Leo, ingawa Yehova anatumia wanaume wasio wakamilifu kuongoza kazi ya kuhubiri na kufundisha, hilo halifanyi tusilitumaini tengenezo la Mungu. Badala yake, tunaimarishwa kwa sababu tunajua kwamba bila msaada wa Yehova, tengenezo halingeweza kufanya mambo linayotimiza. Kupitia hali nyingi ngumu na mambo ambayo amejionea, mtumwa mwaminifu amedhihirisha kwamba roho ya Mungu inaongoza mambo. Sehemu inayoonekana ya tengenezo la Yehova imepata baraka nyingi. Kwa hiyo, tunaiunga mkono kikamili na kuitumaini kabisa.

      JINSI TUNAVYOIUNGA MKONO

      12 Wale ambao wamepewa majukumu kutanikoni wanaonyesha kwamba wanaunga mkono wale wanaoongoza kwa kukubali na kutimiza kwa uaminifu majukumu yao. (Mdo. 20:28) Tukiwa watangazaji wa Ufalme, tunashiriki kwa bidii katika kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba, kufanya ziara za kurudia, na kuongoza mafunzo ya Biblia. (Mt. 24:14; 28:19, 20) Ili tufaidike kikamili na chakula kingi cha kiroho kinachotayarishwa na mtumwa mwaminifu, tunajitayarisha na kuhudhuria mikutano na makusanyiko ya Kikristo. Sisi hufaidika sana kwa kutiana moyo tunaposhirikiana kwa uhuru na ndugu zetu katika mikutano na makusanyiko hayo ya Kikristo.—Ebr. 10:24, 25.

      13 Tunapotoa vitu vyetu vya kimwili ili kuunga mkono tengenezo, tunaonyesha kwamba tunalitumaini kabisa. (Met. 3:9, 10) Tunapoona kwamba ndugu zetu wana uhitaji wa kimwili, tunawasaidia bila kukawia. (Gal. 6:10; 1 Tim. 6:18) Tunafanya hivyo kwa roho ya upendo wa kindugu, tukiwa macho sikuzote ili kuonyesha kwamba tunamshukuru Yehova na tengenezo lake kwa sababu ya wema ambao ametuonyesha.—Yoh. 13:35.

      14 Njia nyingine ambayo tunaonyesha kwamba tunaunga mkono tengenezo ni kwa kukubali maamuzi yanayofanywa. Hilo linatia ndani kufuata kwa unyenyekevu mwongozo wa ndugu waliowekwa rasmi, kama vile waangalizi wa mzunguko na wazee wa makutaniko. Ndugu hao ni miongoni mwa “wale wanaoongoza” ambao tunapaswa kuwatii na kuwanyenyekea. (Ebr. 13:7, 17) Ingawa huenda tusielewe kikamili sababu ya maamuzi fulani, tunajua kwamba tukiyaunga mkono, tutapata faida za kudumu. Matokeo ni kwamba Yehova hutubariki tunapotii Neno lake na tengenezo lake. Kwa kufanya hivyo, tunaonyesha kwamba tunamtii Bwana wetu, Yesu Kristo.

      15 Naam, tuna sababu nyingi za kumtumaini mtumwa mwaminifu na mwenye busara. Shetani, mungu wa mfumo huu wa mambo, anajitahidi juu chini kulivunjia heshima jina la Yehova na tengenezo lake. (2 Kor. 4:4) Usijiruhusu kamwe unaswe na mbinu zenye uovu za Shetani! (2 Kor. 2:11) Anajua kwamba ana “kipindi kifupi cha wakati” kabla hajatupwa ndani ya abiso, naye ameazimia kuwapotosha Wakristo wengi iwezekanavyo wamwasi Mungu. (Ufu. 12:12) Hata hivyo, kadiri Shetani anavyozidisha jitihada zake, na tuendelee kumkaribia Yehova zaidi. Acheni tuendelee kumtumaini Yehova na njia anayotumia kuwaelekeza watu wake leo. Tukifanya hivyo, tutakuwa na undugu wenye umoja.

  • Mipango na Usimamizi Katika Kutaniko
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • SURA YA 4

      Mipango na Usimamizi Katika Kutaniko

      KATIKA barua yake ya kwanza kwa Wakorintho, mtume Paulo alieleza kweli muhimu kumhusu Mungu. Aliandika hivi: “Mungu si Mungu wa machafuko, bali ni wa amani.” Kisha, akieleza zaidi kuhusu mikutano ya kutaniko, alisema hivi: “Mambo yote na yatendeke kwa adabu na kwa mpango.”—1 Kor. 14:33, 40.

      2 Mwanzoni mwa barua hiyohiyo, mtume Paulo alionya kuhusu ugomvi uliokuwa katika kutaniko la Korintho. Paulo aliwahimiza akina ndugu ‘waseme kwa upatano’ na ‘waunganishwe kabisa katika akili ileile na njia ileile ya kufikiri.’ (1 Kor. 1:10, 11) Kisha aliwashauri kuhusu mambo mbalimbali yaliyokuwa yakivuruga umoja wa kutaniko. Akitumia mfano wa mwili wa mwanadamu, alionyesha uhitaji wa kuwa na umoja na ushirikiano. Aliwahimiza washiriki wote wa kutaniko la Kikristo, haidhuru walikuwa na majukumu gani, watunzane kwa upendo. (1 Kor. 12:12-26) Ushirikiano mzuri miongoni mwa wale walio kutanikoni unadhihirisha kwamba kutaniko lingekuwa limepangwa vizuri.

      3 Hata hivyo, kutaniko la Kikristo lilipaswa kuwa na mpangilio gani? Ni nani ambaye angelipanga? Lingekuwa na muundo gani? Ni nani wangepewa majukumu? Biblia inajibu maswali hayo.—1 Kor. 4:6.

      MPANGILIO WA KITHEOKRASI

      4 Kutaniko la Kikristo lilianzishwa katika siku ya Pentekoste mwaka wa 33 W.K. Tunajifunza nini kuhusu kutaniko hilo la karne ya kwanza? Lilipangwa na kusimamiwa kitheokrasi, yaani, lilikuwa chini ya utawala wa Mungu (Kigiriki, the·osʹ na kraʹtos). Maneno hayo mawili ya Kigiriki yanapatikana kwenye 1 Petro 5:10, 11. Masimulizi ya Biblia kuhusu mambo yaliyotendeka Yerusalemu karibu miaka 2,000 iliyopitia yanathibitisha wazi kwamba kutaniko hilo la Wakristo watiwa-mafuta lilianzishwa na Mungu. (Mdo. 2:1-47) Lilikuwa jengo lake, nyumba yake. (1 Kor. 3:9; Efe. 2:19) Leo, kutaniko la Kikristo linafuata utaratibu na mpangilio ambao ulianzishwa katika karne ya kwanza.

      Leo, kutaniko la Kikristo linafuata utaratibu na mpangilio ambao ulianzishwa katika karne ya kwanza

      5 Kutaniko la mapema lilianza na wanafunzi 120 hivi. Andiko la Yoeli 2:28, 29 lilitimizwa wakati roho takatifu ilipomiminwa juu ya wanafunzi hao. (Mdo. 2:16-18) Hata hivyo siku hiyohiyo, karibu watu wengine 3,000 walibatizwa katika maji na kujiunga na kutaniko hilo la watiwa-mafuta. Walikuwa wamekubali ujumbe kumhusu Kristo nao “wakaendelea kujitoa kwa bidii kwa fundisho la mitume.” Kisha, “Yehova akaendelea kuwaongezea kila siku watu waliokuwa wakiokolewa.”—Mdo. 2:41, 42, 47.

      6 Kulikuwa na ongezeko kubwa katika kutaniko la Yerusalemu hivi kwamba kuhani mkuu wa Wayahudi akalalamika kuwa wanafunzi walijaza Yerusalemu fundisho lao. Makuhani wengi Wayahudi walikuwa miongoni mwa wanafunzi wapya waliojiunga na kutaniko huko Yerusalemu.—Mdo. 5:27, 28; 6:7.

      7 Yesu alisema: “Mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika Yudea yote na Samaria, na mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.” (Mdo. 1:8) Na hivyo ndivyo ilivyokuwa, mateso makali yalipotokea Yerusalemu baada ya kifo cha Stefano, wanafunzi waliokuwa wakiishi huko walitawanyika katika eneo lote la Yudea na Samaria. Lakini popote walipoenda, waliendelea kutangaza habari njema na kuwafundisha watu wengi zaidi, kutia ndani baadhi ya Wasamaria. (Mdo. 8:1-13) Baadaye, habari njema ilihubiriwa kwa watu wa mataifa ambao hawakuwa wametahiriwa, yaani, wale ambao hawakuwa Wayahudi. (Mdo. 10:1-48) Kwa sababu ya kazi hiyo kubwa ya kuhubiri watu wengi walikubali kuwa wanafunzi na makutaniko mapya yakaanzishwa nje ya Yerusalemu.—Mdo. 11:19-21; 14:21-23.

      8 Ni mipango gani iliyofanywa ili kuhakikisha kwamba kila kutaniko jipya lililoanzishwa lilipangwa na kusimamiwa kitheokrasi? Kupitia mwongozo wa roho ya Mungu mpango wa kuwa na wachungaji wa kutunza kundi ulianzishwa. Katika safari yao ya kwanza ya umishonari, Paulo na Barnaba waliwaweka rasmi wazee kwenye makutaniko waliyoyatembelea. (Mdo. 14:23) Mwandishi wa Biblia, Luka, anasimulia kuhusu mkutano ambao mtume Paulo alifanya pamoja na wazee wa kutaniko la Efeso. Paulo aliwaambia: “Jiangalieni wenyewe na kundi lote, ambalo kati yake roho takatifu imewaweka ninyi rasmi muwe waangalizi, mlichunge kutaniko la Mungu, ambalo alilinunua kwa damu ya Mwana wake mwenyewe.” (Mdo. 20:17, 28) Walistahili kuwa wazee kwa sababu walitimiza matakwa ya Kimaandiko. (1 Tim. 3:1-7) Tito, mfanyakazi mwenzi wa Paulo alipewa mamlaka ya kuwaweka rasmi wazee katika makutaniko ya Krete.—Tito 1:5.

      9 Makutaniko mengi zaidi yalipoendelea kuanzishwa, mitume na wazee waliokuwa Yerusalemu waliendelea kutumikia wakiwa waangalizi wakuu wa kutaniko la Kikristo la duniani pote katika karne ya kwanza. Walitumikia wakiwa baraza linaloongoza.

      10 Alipoliandikia kutaniko la Efeso, mtume Paulo alieleza kwamba kutaniko la Kikristo lingedumisha umoja na kuendelea kujitiisha chini ya ukichwa wa Yesu Kristo ikiwa tu lingetii mwongozo wa roho ya Mungu. Mtume huyo aliwahimiza Wakristo wa Efeso wasitawishe unyenyekevu na kudumisha “roho ya umoja” wakishirikiana kwa amani na wote walio kutanikoni. (Efe. 4:1-6) Kisha akanukuu Zaburi 68:18 na kuonyesha jinsi ambavyo Yehova aliandaa wanaume wenye sifa za kiroho zilizowastahilisha kushughulikia mahitaji ya kutaniko wakiwa mitume, manabii, waeneza-injili, wachungaji, na walimu. Wanaume hao, wakiwa zawadi kutoka kwa Yehova, wangeimarisha kutaniko zima lifikie ukomavu wa kiroho na kumpendeza Mungu.—Efe. 4:7-16.

      MAKUTANIKO YANAFUATA MFANO WA MITUME

      11 Leo, utaratibu kama huo wa tengenezo unafuatwa katika makutaniko yote ya Mashahidi wa Yehova. Makutaniko hayo yote hufanyiza kutaniko la ulimwenguni

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki