-
Mababa wa Kimitume—Je, Kweli Walifuata Mafundisho ya Mitume?Mnara wa Mlinzi—2009 | Julai 1
-
-
Pia, katika kipindi hicho waandikaji wengine wasiojulikana waliandika vitabu vilivyoitwa The Didache,
-
-
Mababa wa Kimitume—Je, Kweli Walifuata Mafundisho ya Mitume?Mnara wa Mlinzi—2009 | Julai 1
-
-
Je, Yalikuwa Mabadiliko Madogo?
Mawazo fulani ya kale yaliyoitwa eti ya “Kikristo” kwa kweli hayakupatana na mafundisho ya Kristo na mitume wake. Kwa mfano, kinyume na maadhimisho ya Mlo wa Jioni wa Bwana yaliyoanzishwa na Yesu, ambayo pia yanaitwa Mlo wa Jioni wa Mwisho, mwandikaji wa kitabu cha The Didache alipendekeza kwamba divai ipitishwe kabla ya mkate. (Mathayo 26:26, 27) Mwandikaji huyo pia alisema kwamba ikiwa maji mengi hayakupatikana ya kuwabatiza watu kwa kuwazamisha, basi ingetosha tu kumwagilia maji kichwani mtu aliyetaka kubatizwa. (Marko 1:9, 10; Matendo 8:36, 38) Kitabu hichohicho kiliwahimiza Wakristo wafuate desturi kama vile kufunga kwa lazima mara mbili kwa juma na kurudia-rudia Sala ya Bwana mara tatu kwa siku.—Mathayo 6:5-13; Luka 18:12.
-