-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Walikuja kutambua kwamba ijapokuwa Yesu alikuja kwanza duniani akiwa mwanadamu katika mwili, wakati wa kurudi kwake angekuwapo bila kuonekana akiwa mtu wa roho. (Yn. 14:19) Walijifunza zaidi kwamba lengo la kurudi kwa Yesu lilikuwa, si kuharibu kila mtu, bali kubariki familia tiifu za dunia. (Gal. 3:8) Russell aliandika: “Tulihisi tumehuzunishwa sana na kosa la Waadventisti wa Pili, ambao walikuwa wakimtarajia Kristo katika mwili, na kufundisha kwamba ulimwengu na vyote vilivyomo isipokuwa Waadventisti wa Pili ungeteketezwa.”
-
-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Unabii Mbalimbali Unaohusu Wakati na Kuwapo kwa Bwana
Asubuhi moja katika Januari 1876, Russell mwenye umri wa miaka 23 alipokea nakala ya jarida la kidini linaloitwa Herald of the Morning. Kutokana na picha katika jalada, yeye angeweza kuona kwamba lilihusiana na Uadventisti. Mhariri, Nelson H. Barbour, wa Rochester, New York, aliamini kwamba lengo la kurudi kwa Kristo si kuharibu familia za dunia bali kuzibariki na kwamba kuja kwake kungekuwa si katika mwili bali akiwa roho. Aa! hilo lilipatana na yale ambayo Russell na washirika wake katika Allegheny walikuwa wameamini kwa muda fulani!b Ingawa hivyo, ajabu ni kwamba Barbour aliamini kutokana na unabii mbalimbali unaohusu wakati wa Kibiblia kwamba Kristo alikuwa tayari yupo (bila kuonekana) na kwamba wakati ulikuwa umefika wa kufanya kazi ya mavuno ya kukusanya “ngano” (Wakristo wa kweli waliojumuika kuwa jamii ya Ufalme).—Mt., sura 13.
Russell alikuwa ameepuka unabii mbalimbali wa Kibiblia unaohusu wakati. Lakini, sasa, yeye alijiuliza: “Je, ingeweza kuwa kwamba unabii mbalimbali unaohusu wakati ambao nilikuwa nimepuuza kwa muda mrefu sana, kwa sababu ya kutumiwa vibaya na Waadventisti, ulikuwa kwa kweli umekusudiwa uonyeshe wakati ambao Bwana angekuwapo bila kuonekana ili kusimamisha Ufalme wake?” Akiwa na kile kiu chake kisichotoshelezeka cha kweli ya Kimaandiko, ilikuwa sharti Russell ajifunze zaidi. Hivyo alipanga kukutana na Barbour katika Philadelphia. Mkutano huo ulithibitisha maafikiano yao juu ya mafundisho kadhaa ya Biblia na kuandaa fursa kwao wajadiliane. “Tulipokutana mara ya kwanza,” Russell akataarifu baadaye, “alikuwa na mengi ya kujifunza kutoka kwangu juu ya ujalivu wa rudisho unaotegemea utoshelevu wa fidia iliyotolewa kwa ajili ya wote, kama vile mimi nilivyokuwa na mengi ya kujifunza kutoka kwake juu ya wakati.” Barbour alifaulu kumsadikisha Russell kwamba kuwapo kusikoonekana kwa Kristo kulikuwa kumeanza katika 1874.c
‘Aazimia Kufanya Kampeni Yenye Juhudi kwa Ajili ya Kweli’
C. T. Russell alikuwa mtu wa masadikisho hakika. Akiwa amesadikishwa kwamba kuwapo kusikoonekana kwa Kristo kulikuwa kumeanza, aliazimia kupiga mbiu ya jambo hilo kwa wengine. Baadaye alisema hivi: “Kujua uhakika wa kwamba tayari tulikuwa katika kipindi cha mavuno kulinipa msukumo wa kueneza Kweli ambao sikuwa nimepata kuwa nao hapo awali. Kwa hiyo niliazimia kufanya kampeni yenye juhudi kwa ajili ya Kweli.” Sasa Russell aliamua kupunguza shughuli zake za kibiashara ili ajitoe mwenyewe afanye kazi ya kuhubiri.
Ili kupinga maoni yoyote yenye kosa kuhusu kurudi kwa Bwana, Russell aliandika kijitabu The Object and Manner of Our Lord’s Return. Kilitangazwa katika 1877. Mwaka huohuo Barbour na Russell walitangaza kwa kushirikiana kitabu Three Worlds, and the Harvest of This World. Kitabu hiki chenye kurasa 196 kilizungumza habari za rudisho na unabii mbalimbaliunaohusu wakati wa Kibiblia. Ingawa kila habari ilikuwa imezungumzwa na wengine awali, katika maoni ya Russell kitabu hiki kilikuwa ndicho “cha kwanza kuunganisha hilo wazo la rudisho na unabii unaohusu wakati.” Kilitoa maoni ya kwamba kuwapo kusikoonekana kwa Yesu Kristo kulianza tarehe ya vuli ya mwaka 1874.
-