Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Iweke Karibu Akilini Siku ya Yehova
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
    • Kutenganishwa kwa Watu

      8. (a) Katika Mathayo 13:24-30, 36-43, Yesu alitaja jambo gani jingine ambalo linahusiana na mwisho wa ulimwengu huu? (b) Mfano wa Yesu wamaanisha nini?

      8 Yesu alitaja mambo mengine muhimu yanayohusiana na mwisho wa ulimwengu huu. Jambo moja ni kutenganishwa kwa “wana wa ufalme” kutoka kwa “wana wa yule mwovu.” Yesu alieleza jambo hilo katika mfano wa adui aliyepanda magugu katikati ya ngano. “Ngano” aliyotaja katika mfano wake yawakilisha Wakristo wa kweli waliotiwa mafuta. “Magugu” ni wale wanaodai kuwa Wakristo lakini wanajithibitisha kuwa “wana wa yule mwovu” kwa sababu wanashikamana mno na ulimwengu ambao unatawaliwa na Ibilisi. Wanatenganishwa kutoka kwa “wana wa ufalme” wa Mungu nao wametiwa alama ya kuangamizwa. (Mathayo 13:24-30, 36-43) Je, utenganishaji huo umefanywa?

      9. (a) Baada ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, wote waliodai kuwa Wakristo walitenganishwaje? (b) Wakristo watiwa-mafuta walithibitishaje kwamba wao ni watumishi waaminifu wa Ufalme?

      9 Baada ya Vita ya Kwanza ya Ulimwengu, wote waliodai kuwa Wakristo walitenganishwa kwenye vikundi viwili: (1) Makasisi wa Jumuiya ya Wakristo na wafuasi wao, ambao waliunga mkono kwa dhati Ushirika wa Mataifa (sasa ni Umoja wa Mataifa) huku wakitetea mataifa yao, na (2) Wakristo wa kweli walioishi baada ya vita hiyo, ambao waliunga mkono kwa dhati Ufalme wa Kimesiya wa Mungu, badala ya kuunga mkono mataifa ya ulimwengu huu. (Yohana 17:16) Walithibitisha kwamba wao ni watumishi waaminifu wa Ufalme wa Mungu kwa kuhubiri “habari njema hii ya ufalme” duniani pote. (Mathayo 24:14) Matokeo yamekuwa nini?

      10. Kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme ilikuwa na matokeo gani kwanza?

      10 Kwanza, mabaki ya wale waliotiwa mafuta kwa roho ya Mungu wenye tumaini la kutawala pamoja na Kristo katika Ufalme wa mbinguni, walianza kukusanywa. Walikusanywa katika tengenezo lenye umoja wajapoishi katika mataifa mbalimbali. Kazi ya kuwatia muhuri watiwa-mafuta inakaribia mwisho.—Ufunuo 7:3, 4.

      11. (a) Ni kazi gani ya kukusanya inayoendelea, na kazi hiyo inatimiza unabii gani? (b) Kutimia kwa unabii huo kunaonyesha nini?

      11 Kisha “umati mkubwa . . . kutoka katika mataifa yote na makabila na vikundi vya watu na lugha,” ulianza kukusanywa chini ya mwelekezo wa Kristo. Hao ni “kondoo wengine” ambao wataokoka “dhiki kubwa” na kuingia katika ulimwengu mpya wa Mungu. (Ufunuo 7:9, 14; Yohana 10:16) Kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme wa Mungu kabla mwisho haujaja ingali inaendelea leo. Kwa uaminifu, umati mkubwa wa kondoo wengine, ambao sasa idadi yao imefikia mamilioni, wanawasaidia mabaki watiwa-mafuta kuhubiri ujumbe muhimu wa Ufalme. Ujumbe huo unahubiriwa katika mataifa yote.

  • Iweke Karibu Akilini Siku ya Yehova
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
    • Kwanza, kutenganishwa kwa watu kuhusiana na suala la Ufalme hakujamalizika bado. Hivi sasa, katika baadhi ya maeneo ambayo yalikuwa na upinzani mkali kwa miaka mingi, watu wengi wameanza kujifunza Biblia. Hata katika sehemu ambazo watu wanakataa habari njema, rehema ya Yehova inaonekana tunapotoa ushahidi. Kwa hiyo, endelea kuhubiri! Yesu anatuhakikishia kwamba mwisho utakuja tukamilishapo kazi hiyo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki