-
Kurudi kwa KristoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kwa upande mwingine, neno la Kigiriki er·khoʹme·non limetumiwa katika andiko la Mathayo 24:30, linalosema kuhusu “Mwana wa binadamu akija [kutimiza kazi aliyopewa na Yehova ya kuwaangamiza waovu kwenye vita vya Har–Magedoni] juu ya mawingu ya mbinguni akiwa na nguvu na utukufu mwingi.” Watafsiri fulani hutumia ‘kuja’ kwa maneno yote mawili ya Kigiriki, lakini wale walio waangalifu zaidi huonyesha tofauti kati ya maneno hayo mawili.
-
-
Kurudi kwa KristoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Biblia inamaanisha nini inaposema kwamba Yesu atakuja “vivyo hivyo” kama alivyopanda mbinguni?
Mdo. 1:9-11: “Huku [mitume wa Yesu] walipokuwa wakitazama, akainuliwa na wingu likamchukua juu kutoka machoni pao. Nao walipokuwa wakitazama angani alipokuwa ameondoka na kwenda, pia, tazama! wanaume wawili wenye mavazi meupe wakasimama kando yao, nao wakasema: ‘Wanaume wa Galilaya, kwa nini mnasimama mkitazama angani? Yesu huyu aliyepokewa juu angani kutoka kwenu atakuja vivyo hivyo kama vile ambavyo mmemwona akienda angani.’” (Ona kwamba andiko hilo linasema “vivyo hivyo,” wala si mwili uleule. Alipanda mbinguni jinsi gani? Kama mstari wa 9 unavyoonyesha, alitoweka machoni pao, na kuondoka kwake kulionwa na wanafunzi wake tu. Ulimwengu kwa ujumla haukujua yaliyokuwa yametukia. Hivyo ndivyo ingekuwa wakati wa kurudi kwa Kristo.)
Maneno “anakuja na mawingu, na kila jicho litamwona” yanamaanisha nini?
Ufu. 1:7: “Tazama! Anakuja na mawingu, na kila jicho litamwona, na wale waliomchoma; na makabila yote ya dunia yatajipiga-piga kwa huzuni kwa sababu yake.” (Ona pia Mathayo 24:30; Marko 13:26; Luka 21:27.)
“Mawingu” yanawakilisha nini? Ni kutoonekana. Wakati ndege inapokuwa katika wingu zito au juu ya mawingu, kwa kawaida watu walio chini hawawezi kuiona, ingawa huenda wakasikia mngurumo wa injini zake. Yehova alimwambia Musa hivi: “Nitakujia katika wingu lenye giza.” Musa hakumwona Mungu, lakini wingu hilo lilionyesha kuwapo kusikoonekana kwa Yehova. (Kut. 19:9; ona pia Mambo ya Walawi 16:2; Hesabu 11:25.) Kama Kristo angetokea akionekana kwa macho mbinguni, ni wazi kwamba si “kila jicho” lingemwona. Kwa mfano, kama angetokea Australia, je, angeonekana Ulaya, Afrika, na Amerika?
“Kila jicho litamwona” jinsi gani? Watatambua kutokana na matukio duniani kwamba yeye yupo ijapokuwa haonekani kwa macho. Pia likielekezea kuona ambako si kwa macho halisi, andiko la Yohana 9:41 linasema hivi: “Yesu akawaambia [Mafarisayo]: ‘Kama mngekuwa vipofu, hamngekuwa na dhambi. Lakini sasa mnasema, “Tunaona.” Dhambi yenu inabaki.’” (Linganisha na Waroma 1:20.) Baada ya kurudi kwa Kristo, watu fulani wanaamini; wanaitambua ishara ya kuwapo kwake. Wengine wanakataa uthibitisho, lakini Kristo atakapoanza kutenda akiwa yule aliyewekwa na Mungu kuwaangamiza waovu, wataona nguvu zake na kutambua kwamba uharibifu huo hautoki kwa wanadamu bali unatoka mbinguni. Watajua linalotukia kwa sababu walikuwa wameonywa mapema. Kwa sababu ya jambo linalowapata, ‘watajipiga-piga kwa kuomboleza.’
“Wale waliomchoma” ni nani? Kihalisi, askari wa Roma ndio waliomchoma Yesu alipouawa. Lakini walikufa zamani. Kwa hiyo, maneno hayo yanamaanisha watu wanaowatendea vibaya jinsi hiyohiyo, au ‘wanaowachoma,’ wafuasi wa kweli wa Kristo wakati wa “siku za mwisho.”—Mt. 25:40, 45.
-
-
Kurudi kwa KristoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Tunapaswa kukumbuka kwamba kuna tofauti kati ya kuja na kuwapo. Kwa hiyo, ingawa kuja kwa mtu (kunakohusianishwa na kufika au kurudi kwake) kunatukia katika wakati fulani, huenda kuwapo kwake baada ya hapo kukaendelea kwa kipindi cha miaka kadhaa. Katika Biblia neno la Kigiriki erʹkho·mai (linalomaanisha “kuja”) linatumiwa pia kumhusu Yesu akielekeza fikira kwenye kazi muhimu katika kipindi hususa wakati wa kuwapo kwake, yaani, kazi yake aliyopewa na Yehova ya kuwaangamiza waovu kwenye vita vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.
-