Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je! Jina Lako Limo Katika Kitabu cha Uhai?
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Kwa hiyo, endelea kukumbuka jinsi wewe umepokea na jinsi wewe ulisikia, na kuzidi kukishika, na kutubu. Kwa hakika usipoamka, mimi nitakuja kama mwivi, na wewe hutajua hata kidogo ni kwenye saa gani mimi nitakuja juu yako wewe.”—Ufunuo 3:2, 3, NW.

  • Je! Jina Lako Limo Katika Kitabu cha Uhai?
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • Kuja “Kama Mwivi”

      6. Yesu alikujaje “kama mwivi” katika 1918, na alikuta hali gani miongoni mwa waliodai kuwa wafuasi wake?

      6 Onyo la Yesu kwamba yeye angekuja “kama mwivi” linafika mpaka ndani ya nyakati za ki-siku-hizi. Lilikuwa na tumizi la pekee kwa Wakristo walioishi mpaka kuingia katika siku ya Bwana. Upesi baada ya 1914, kulikuwako utimizo wa unabii wa Malaki: “‘Kwa ghafula Bwana wa kweli atakuja kwenye hekalu Lake, ambaye nyinyi watu mnatafuta, na mjumbe wa agano ambaye katika yeye nyinyi mnapendezwa. Tazama! Yeye atakuja kwa hakika,’ Yehova wa majeshi amesema.” (Malaki 3:1, NW; Ufunuo 1:10) Akiwa “mjumbe wa agano,” Yesu alikuja kukagua na kuhukumu wale waliodai kuwa wafuasi wake. (1 Petro 4:17) Wakati huo, katika 1918, Jumuiya ya Wakristo ilikuwa imejitia katika umwagaji-damu katika Vita ya Ulimwengu 1, na ilikuwa mfu kabisa, kiroho. Hata Wakristo wa kweli, ambao kabla ya vita walikuwa wamehubiri kwa bidii, walipitia wakati wa lepe la usingizi wa kiroho. Baadhi ya wazee wao mashuhuri walitiwa gerezani, na utendaji wa kuhubiri ukakaribia kukoma. Wakati roho ya Yehova ilipoamsha Wakristo hawa mwaka uliofuata, si wote waliokuwa tayari. Baadhi yao, kama wale wanawali wapumbavu wa mfano wa Yesu, hawakutayarishwa kwa vifaa kiroho kwa ajili ya pendeleo la kumtumikia Yehova. Hata hivyo, kwa furaha, walikuwako wengi ambao, kama wale wanawali waangalifu, walikuwa wametii onyo la Yesu: “Fulizeni kulinda, basi, kwa sababu nyinyi hamjui wala siku yenyewe wala saa yenyewe.”—Mathayo 25:1-13, NW.

      7. Ni kwa nini Wakristo leo wanahitaji kukaa hali wameamka?

      7 Uhitaji wa Mkristo kuendelea kuwa chonjo haukumalizika mapema katika siku ya Bwana. Katika unabii wake mkubwa kuhusu “ile ishara wakati mambo yote haya yamekusudiwa kuja kwenye umalizio,” Yesu alitoa onyo lenye mkazo: “Kuhusu siku hiyo au saa hakuna mtu anayejua . . . Fulizeni kutazama, fulizeni kuamka, kwa maana nyinyi hamjui wakati uliowekwa ni lini. Lakini kitu ninachoambia nyinyi ninaambia wote, fulizeni kulinda.” (Marko 13:4, 32, 33, 37, NW) Ndiyo, mpaka saa ii hii, kila mmoja wetu, awe ni wa wapakwa-mafuta au wa ule umati mkubwa, anahitaji kukaa chonjo na kupiga vita dhidi ya kupeperushwa kuingia ndani ya usingizi wa kiroho. Siku ya Yehova ijapo ‘kama mwivi usiku,’ sisi na tupatikane tukiwa tumeamka kabisa ili tupokee hukumu yenye upendeleo.—1 Wathesalonike 5:2, 3; Luka 21:34-36, NW; Ufunuo 7:9.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki