-
Je, Kutahiriwa Ni Ishara ya Kuwa Mtu Mzima?Mnara wa Mlinzi—2007 | Juni 1
-
-
Hata hivyo, katika mataifa mengine, sherehe ya kutahiriwa inafanywa mtoto wa kiume anapokuwa mtu mzima. Kwa kawaida, hilo linatia ndani kumpeleka jandoni, yaani, shule ya kitamaduni, ambako anatahiriwa na kutengwa na jamii kwa majuma fulani mpaka apone. Wakati huo, mtoto huyo anapaswa kufuata desturi fulani naye anafundishwa kuwa mwanamume. Je, ni lazima mtoto wa kiume atahiriwe hivyo ili kuthibitisha kwamba sasa yeye ni mtu mzima? Acheni tuchunguze yale ambayo Biblia inasema kuhusu maoni ya Mungu kuelekea jambo hilo.—Methali 3:5, 6.
-
-
Je, Kutahiriwa Ni Ishara ya Kuwa Mtu Mzima?Mnara wa Mlinzi—2007 | Juni 1
-
-
Namna Gani “Elimu ya Jando”?
Namna gani wazazi Wakristo wakiamua watoto wao wa kiume watahiriwe? Je, wangekuwa wakitenda kupatana na Biblia ikiwa wangeamua kuwapeleka wana wao kwa ile inayoitwa eti elimu ya jando iliyotajwa mapema? Kwenda jandoni kunatia ndani mambo mengi zaidi ya kukata tu magovi. Kwa majuma kadhaa, yule anayeenda jandoni ataishi na kushirikiana kwa ukaribu na vijana na walimu ambao hawamwabudu Yehova. Mambo mengi yanayofundishwa katika jando yanapingana na viwango vya juu vya maadili vya Biblia. Biblia inaonya hivi: “Mashirika mabaya huharibu tabia nzuri.”—1 Wakorintho 15:33.
Pia, hatari za kimwili zinazoweza kumpata mtu anayeenda jandoni zinazidi kuongezeka. Mwaka wa 2003, gazeti moja (South African Medical Journal) lilionya hivi: “Matokeo yenye kutisha ya kutahiriwa yameonekana tena mwaka huu. Ripoti nyingi za vifo na madhara mengine ya kukatwa vibaya viungo vya uzazi zinatangazwa ulimwenguni pote na mashirika makubwa ya habari. . . . Kwa ufupi, nyingi kati ya zile zinazoitwa eti ‘shule za kutahiri’ au jando, leo ni bandia na hatari.”
Zaidi ya hatari ya kijana kuumizwa vibaya kimwili, kuna hatari kubwa hata zaidi ya kiroho. Mafundisho na mambo yanayofanywa jandoni yanahusiana sana na kuwasiliana na pepo na ibada ya mababu waliokufa. Kwa mfano, badala ya kukubali kwamba madaktari wasio waangalifu na hali zisizo safi kiafya zinasababisha madhara, wengi wanaamini kwamba misiba hiyo inasababishwa na ulozi au hasira ya mababu waliokufa. Biblia inatoa amri hii kuhusu kushirikiana na dini ya uwongo: “Msifungwe nira isivyo sawa pamoja na wasio waamini. Kwa maana kuna ushirika gani kati ya uadilifu na uasi-sheria? Au nuru ina ushirika gani na giza? . . . ‘Kwa hiyo tokeni katikati yao, na mjitenge,’ asema Yehova, ‘na mwache kugusa kitu kilicho najisi’; ‘nami nitawakaribisha ndani.’” (2 Wakorintho 6:14-17) Kulingana na shauri hilo, halingekuwa jambo la hekima kwa wazazi Wakristo kuwapeleka watoto wao wa kiume katika jando.
-