-
Mwisho wa Enzi—Je, Ni Tumaini kwa Wakati Ujao?Amkeni!—1996 | Julai 8
-
-
Kwa wakati uo huo, yale mataifa mawili makuu, Muungano wa Sovieti na Marekani, yalikuwa yakifanya maendeleo makubwa katika kupunguza majeshi na kuondoa tisho la nyuklia. Kila mwafaka uliofanywa ulitokeza tumaini jipya kwamba amani ya ulimwengu ingeweza kupatikana—hivi kwamba mwandikaji John Elson akasema hivi Septemba 1989: “Siku za mwisho za miaka ya 1980, kwa wafafanuzi wengi wa mambo, ni za kuaga silaha kwa njia fulani. Vita baridi yaonekana kama imekwisha; amani inaonekana inatokea katika sehemu nyingi za ulimwengu.”
-
-
Mwisho wa Enzi—Je, Ni Tumaini kwa Wakati Ujao?Amkeni!—1996 | Julai 8
-
-
Kumaliza Vita Baridi
Mtungaji wa vitabu Selbourne asema: “Mwendo wa ujumla wa kuanguka kwa Ulaya mashariki ulifuatana kwa njia ya kustaajabisha.” Kisha aongezea: “Kwa wazi kichocheo kilikuwa kutwaa mamlaka kwa Gorbachev katika Moscow mnamo Machi 1985 na kumaliza kwake ‘Sera ya Brezhnev’, jambo ambalo lilinyima tawala za Ulaya mashariki uhakikisho wa kupata msaada wa Sovieti na wa kuingiliwa mambo iwapo maasi ya wengi yangetokea.”
Gorbachev atajwa na The New Encyclopædia Britannica kuwa “mwanzilishi wa pekee kabisa wa mfululizo wa matukio mwishoni-mwishoni mwa 1989 na 1990 ambao ulibadili mfumo wa kisiasa wa Ulaya na kuanzisha kumalizika kwa Vita Baridi.”
Bila shaka, Gorbachev hangeweza kumaliza Vita Baridi akiwa peke yake. Akionyesha mambo ambayo yangetukia karibuni, waziri mkuu wa Uingereza Margaret Thatcher alisema hivi baada ya kukutana naye kwa mara ya kwanza: “Nampenda Bwa. Gorbachev. Tunaweza kushirikiana.” Na zaidi, uhusiano wa kibinafsi na wa kipekee kati ya Thatcher na rais wa Marekani Reagan ulimwezesha Thatcher amsadikishe Reagan kwamba ni jambo la hekima kushirikiana na Gorbachev. Gail Sheehy, mtungaji wa kitabu Gorbachev—The Making of the Man Who Shook the World, akata kauli hivi: “Thatcher angeweza kufurahi kuwa ‘katika maana halisi yeye alikuwa mdhamini wa uhusiano kati ya Reagan na Gorbachev.’”
Na kama vile mara nyingi imetukia katika historia, watu muhimu walikuwa mahali pafaapo kwa wakati ufaao ili kuleta mabadiliko ambayo labda hayangetokea.
-