Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Huruma Nyororo ya Mungu Wetu”
    Mkaribie Yehova
    • Kwa mfano, fikiria kitenzi cha Kiebrania ra·chamʹ, ambacho mara nyingi hutafsiriwa “onyesha rehema” au “hurumia.” Kichapo kimoja cha marejeo kinaeleza kwamba kitenzi ra·chamʹ “kinaonyesha huruma nyingi na yenye upendo, kama ile tunayohisi tunapowaona wapendwa wetu au wale wanaohitaji msaada wetu wakiteseka au kuumia.” Neno hilo la Kiebrania, ambalo Yehova anatumia kujihusu, linahusiana na neno linalomaanisha “tumbo la uzazi” nalo linaweza kufasiriwa kuwa “huruma ya mama.”a—Kutoka 33:19; Yeremia 33:26.

  • “Huruma Nyororo ya Mungu Wetu”
    Mkaribie Yehova
    • Huruma Ni Nini?

      3. Kitenzi cha Kiebrania kinachotafsiriwa “onyesha rehema” au “hurumia” kinamaanisha nini?

      3 Katika Biblia, huruma na rehema zinahusiana sana. Maneno kadhaa ya Kiebrania na Kigiriki yanadokeza sifa ya huruma yenye upendo. Kwa mfano, fikiria kitenzi cha Kiebrania ra·chamʹ, ambacho mara nyingi hutafsiriwa “onyesha rehema” au “hurumia.” Kichapo kimoja cha marejeo kinaeleza kwamba kitenzi ra·chamʹ “kinaonyesha huruma nyingi na yenye upendo, kama ile tunayohisi tunapowaona wapendwa wetu au wale wanaohitaji msaada wetu wakiteseka au kuumia.” Neno hilo la Kiebrania, ambalo Yehova anatumia kujihusu, linahusiana na neno linalomaanisha “tumbo la uzazi” nalo linaweza kufasiriwa kuwa “huruma ya mama.”a—Kutoka 33:19; Yeremia 33:26.

      Mama akiwa amembeba mtoto wake huku akimtazama kwa upendo

      “Je, mwanamke aweza kumsahau . . . mwana wa tumbo lake? ”

      4, 5. Biblia inatumiaje hisia ambazo mama huwa nazo kwa mtoto wake mchanga kutufundisha kuhusu huruma ya Yehova?

      4 Biblia inatumia hisia ambazo mama huwa nazo kwa mtoto wake mchanga kutufundisha maana ya huruma ya Yehova. Twasoma hivi kwenye Isaya 49:15: “Je! mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyaye, hata asimhurumie [ra·chamʹ] mwana wa tumbo lake? naam, hawa waweza kusahau, lakini mimi sitakusahau wewe.” Maelezo hayo yenye kugusa moyo yanakazia jinsi Yehova alivyo na huruma nyingi kwa watu wake. Jinsi gani?

      5 Ni vigumu kuwazia kwamba mama anaweza kusahau kumnyonyesha na kumtunza mtoto wake mchanga. Kwani, mtoto mchanga ni hoi; anahitaji kupendwa na kutunzwa na mama yake usiku na mchana. Ingawa hivyo, inasikitisha kupata habari kuhusu akina mama wanaowatupa watoto wao, hasa katika ‘nyakati hizi za hatari’ kwa sababu watu hawana “shauku ya kiasili.” (2 Timotheo 3:1, 3) “Lakini mimi sitakusahau wewe,” atangaza Yehova. Yehova hakosi kamwe kuwaonyesha watumishi wake huruma nyororo. Huruma hiyo ni yenye nguvu zaidi ya hisia yenye nguvu tunayoweza kuwazia, yaani, huruma ambayo kwa kawaida mama humwonyesha mtoto wake mchanga. Haishangazi kwamba mtoa-maoni mmoja alisema hivi kuhusu Isaya 49:15: “Hili ni mojawapo, au ndilo neno linalofafanua upendo wa Mungu waziwazi zaidi katika Agano la Kale.”

      6. Wanadamu wengi wasiokamilika wamekuwa na maoni gani kuhusu huruma nyororo, lakini Yehova anatuhakikishia nini?

      6 Je, kuwa na huruma nyororo ni udhaifu? Wanadamu wengi wasiokamilika wamekuwa na maoni hayo. Kwa mfano, mwanafalsafa Mroma Seneca, msomi maarufu wa Roma ambaye aliishi wakati wa Yesu, alifundisha kwamba “huruma ni udhaifu wa akili.” Seneca aliunga mkono Ustoiki, falsafa inayokazia kuwa na utulivu bila hisia zozote. Mtu mwenye hekima anaweza kuwasaidia wale wanaotaabika, akasema Seneca, lakini hapaswi kuwahurumia kwa sababu atakosa utulivu akifanya hivyo. Maoni hayo ya ubinafsi kuhusu maisha yaliwazuia watu wasionyeshe huruma kutoka moyoni. Lakini sivyo alivyo Yehova! Yehova anatuhakikishia katika Neno lake kwamba yeye “ni mwenye wororo sana katika shauku na mwenye rehema [kihalisi, “mwenye huruma”].” (Yakobo 5:11) Kama tutakavyoona, kuonyesha huruma si udhaifu bali ni sifa muhimu sana yenye nguvu.

  • “Huruma Nyororo ya Mungu Wetu”
    Mkaribie Yehova
    • a Hata hivyo, kwenye Zaburi 103:13, kitenzi cha Kiebrania ra·chamʹ kinamaanisha rehema, au huruma, ambayo baba huwaonyesha watoto wake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki