Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Muda mfupi baada ya kuoa, Martin Poetzinger alikamatwa na kupelekwa kwenye kambi yenye sifa mbaya ya Dachau, kisha katika Mauthausen. Mke wake, Gertrud, alifungwa katika Ravensbrück. Hawakuonana kwa miaka tisa. Akikumbuka mambo aliyoona katika Mauthausen, aliandika hivi baadaye: “Gestapo walijaribu kila njia ili kutushawishi tuvunje imani yetu katika Yehova. Kunyimwa chakula, urafiki wa hila, ukatili, kusimama siku baada ya siku katika fremu, kuangikwa juu ya nguzo ya meta 3 kwa viwiko vilivyozungushwa nyuma, kuchapwa viboko—yote hayo na mengine ya aibu sana kuweza kutajwa yaliweza kujaribiwa.”

  • “Vitu vya Kuchukiwa na Mataifa Yote”
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Sanduku katika ukurasa wa 660]

      “Wanyanyaswa kwa Sababu za Kidini”

      “Kulikuwa na kikundi cha watu katika Kambi ya Mateso ya Mauthausen walionyanyaswa kwa sababu za kidini tu: washiriki wa farakano liitwalo ‘Wanafunzi wa Biblia Wenye Bidii,’ au ‘Mashahidi wa Yehova’ . . . Kukataa kwao kula kiapo cha uaminifu-mshikamanifu kwa Hitler na kukataa kwao kutoa aina yoyote ya utumishi wa kijeshi—likiwa tokeo la itikadi yao kuhusu siasa—ndiyo iliyokuwa sababu ya kunyanyaswa kwao.”—“Die Geschichte des Konzentrationslagers Mauthausen” (Historia ya Kambi ya Mateso ya Mauthausen), iliyotungwa na Hans Maršálek, Vienna, ­Austria, 1974.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki