Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote
    2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Baadaye, bila kujua lolote kuhusu Edvard, ofisi ya tawi iliwatuma mapainia wa pekee wa muda huko Mossaka kwa miezi mitatu. Siku mbili tu kabla waondoke huko, Daniel, mmoja wa mapainia hao wa pekee, alimwona Edvard akiongoza funzo la Biblia kwa kutumia broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Kwa hiyo, Daniel akamfikia Edvard na kuzungumza naye. Edvard akamwambia: “Ninahubiri. Mimi ni mhubiri. Unaweza kumuuliza baba yangu.” Daniel alikutana na baba ya Edvard ambaye alimhakikishia kuwa mambo aliyosema Edvard yalikuwa ya kweli. Mapainia hao wa pekee wa muda walitumia siku mbili zilizosalia kabla ya kumaliza mgawo ili kumzoeza Edvard katika huduma. Baada ya wao kuondoka, Edvard aliendelea kuhubiri kwa bidii, na kuongoza zaidi ya mafunzo kumi ya Biblia. Pia alijiweka wakfu kwa Yehova.

  • Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote
    2012 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Hivi majuzi, painia wa pekee alitumwa katika eneo hilo. Mwezi wa Aprili, Edvard—ambaye wakati huo alikuwa painia msaidizi—pamoja na painia huyo wa pekee, waliwakaribisha watu 182 waliopendezwa kwenye Ukumbusho. Edvard ana mafunzo 16, na 7 kati yao wanahudhuria mikutano ambayo inaongozwa na ndugu hao wawili.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki