Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mikutano ‘Inayotuchochea Katika Upendo na Matendo Mazuri’
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • ubatizo. Makusanyiko husaidia sana kuwaimarisha watu ili wakue kiroho. Makusanyiko huthibitisha kwamba watu wa Yehova ni undugu wa kimataifa wa Wakristo waliojiweka wakfu ambao wana alama inayowatambulisha kuwa wanafunzi wa Yesu Kristo.—Yoh. 13:35.

      27 Tunapohudhuria mikutano ya kutaniko na makusanyiko ya watu wa Yehova, tunaimarishwa ili tufanye mapenzi ya Yehova. Pia, tunalindwa dhidi ya mtazamo wa ulimwengu unaoweza kudhoofisha imani yetu ya Kikristo. Mikutano hiyo yote humletea Yehova sifa na utukufu. (Zab. 35:18; Met. 14:28) Tunathamini kwamba Yehova ameandaa pindi hizo za kuwaburudisha kiroho watu wake waliojiweka wakfu katika nyakati hizi za mwisho.

      MLO WA JIONI WA BWANA

      28 Mara moja kila mwaka, makutaniko yote ya Mashahidi wa Yehova huadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Kristo, au Mlo wa Jioni wa Bwana. (1 Kor. 11:20, 23, 24) Huo ndio mkutano muhimu zaidi wa watu wa Yehova katika mwaka. Tumeagizwa waziwazi tuadhimishe Ukumbusho huo.—Luka 22:19.

      29 Tarehe ya Ukumbusho hulingana na tarehe ya Pasaka inayotajwa katika Biblia. (Kut. 12:2, 6; Mt. 26:17, 20, 26) Pasaka ilikuwa mwadhimisho wa kila mwaka ambao uliwakumbusha Waisraeli siku waliyotoka Misri, mwaka wa 1513 K.W.K. Wakati huo, Yehova alichagua siku ya 14 ya mwezi wao wa kwanza kuwa tarehe ambayo wangemla mwana-kondoo wa Pasaka na kutoka utumwani Misri. (Kut. 12:1-51) Tarehe hiyo hupatikana kwa kuhesabu siku 13 kuanzia wakati mwezi mpya unapoonekana huko Yerusalemu, karibu Machi 21 hivi. Kwa kawaida, kila mwaka mwadhimisho wa Ukumbusho huangukia tarehe ambayo mwezi mpevu huonekana kwa mara ya kwanza baada ya Machi 21.

      30 Andiko la Mathayo 26:26-28 linataja maneno ya Yesu kuhusu jinsi Ukumbusho unavyopaswa kuadhimishwa. Ukumbusho si desturi yenye mafumbo, bali ni mlo wa mfano ambao unaliwa na wale waliochaguliwa kuwa warithi pamoja na Yesu Kristo katika Ufalme wake wa mbinguni. (Luka 22:28-30) Wakristo wengine wote waliojiweka wakfu na watu wanaopendezwa hutiwa moyo kuhudhuria Mlo wa Jioni wa Bwana wakiwa watazamaji. Wanapohudhuria, wanaonyesha kwamba wanathamini maandalizi ambayo Yehova Mungu amefanya kupitia Mwanaye, Yesu Kristo, kwa faida ya wanadamu wote. Kabla ya Ukumbusho, hotuba ya pekee ya watu wote hutolewa ili kuwafanya watu watazamie kwa hamu tukio hilo na kuwachochea wanaopendezwa wajifunze Biblia.

      31 Mashahidi wa Yehova hutazamia kwa hamu pindi za kukusanyika pamoja kwenye mikutano, ambako ‘tunafikiriana ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri.’ (Ebr. 10:24) Mtumwa mwaminifu na mwenye busara huwa macho ili kupanga mikutano hiyo kulingana na mahitaji yetu ya kiroho. Watumishi wote wa Yehova pamoja na watu wote wanaopendezwa wanahimizwa kuthamini sana mpango wa kukusanyika pamoja kwa ukawaida. Watumishi wa Mungu huunganishwa kwa umoja wanapothamini maandalizi ambayo Yehova anafanya kupitia tengenezo lake. Jambo muhimu zaidi, tunamsifu na kumtukuza Yehova.—Zab. 111:1.

  • Wahudumu wa Habari Njema
    Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova
    • SURA YA 8

      Wahudumu wa Habari Njema

      YEHOVA alimtuma Mwanaye, Yesu Kristo, ili atuwekee kielelezo bora cha kuiga. (1 Pet. 2:21) Mtu anapokuwa mfuasi wa Yesu, anahubiri habari njema akiwa mhudumu wa Mungu. Akionyesha kwamba jambo hilo lingeburudisha kiroho, Yesu alisema: “Njooni kwangu, nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo, nami nitawaburudisha. Chukueni nira yangu na mjifunze kutoka kwangu, kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu moyoni, nanyi mtapata burudisho kwa ajili yenu.” (Mt. 11:28, 29) Wote ambao wamekubali mwaliko huo wameona ahadi hiyo ikitimia!

      2 Akiwa Mhudumu Mkuu wa Mungu, Yesu alichagua watu fulani wawe wafuasi wake. (Mt. 9:9; Yoh. 1:43) Aliwazoeza katika huduma na kuwatuma wafanye kazi ileile aliyokuwa akifanya. (Mt. 10:1–11:1; 20:28; Luka 4:43) Baadaye aliwatuma wengine 70 wakatangaze habari njema ya Ufalme wa Mungu. (Luka 10:1, 8-11) Yesu alipowatuma wanafunzi wake, aliwaambia hivi: “Yeyote anayewasikiliza ninyi ananisikiliza mimi pia. Na yeyote anayewapuuza ninyi ananipuuza mimi pia. Isitoshe, yeyote anayenipuuza mimi anampuuza pia Yule aliyenituma.” (Luka 10:16) Kwa kusema hivyo, Yesu alikazia jukumu zito alilowapa wanafunzi wake. Walipaswa kumwakilisha Yesu na Mungu Aliye Juu Zaidi! Ndivyo ilivyo leo kwa wale wanaokubali mwaliko huu wa Yesu: Njoo “uwe mfuasi wangu.” (Luka 18:22; 2 Kor. 2:17) Mungu anawapa wale wanaokubali mwaliko huo utume wa kuhubiri habari njema ya Ufalme na kufundisha.—Mt. 24:14; 28:19, 20.

      3 Kwa kuwa tumekubali mwaliko wa Yesu na kumfuata, tumebarikiwa ‘kumjua’ Yehova Mungu na Yesu Kristo. (Yoh. 17:3) Tumefundishwa njia za Yehova. Ametusaidia kufanya upya akili yetu, kuvaa utu mpya, na kupatanisha maisha yetu na viwango vyake vya uadilifu. (Rom. 12:1, 2; Efe. 4:22-24; Kol. 3:9, 10) Kwa kuwa tunathamini mambo hayo kutoka moyoni, tumechochewa tujiweke wakfu kwa Yehova na kuonyesha wakfu huo kwa kubatizwa katika maji. Tunapobatizwa tunakuwa wahudumu waliowekwa rasmi.

      4 Sikuzote kumbuka kwamba tunapaswa kumtumikia Mungu tukiwa na mikono isiyo na hatia na moyo safi. (Zab. 24:3, 4; Isa. 52:11; 2 Kor. 6:14–7:1) Kupitia imani katika Yesu Kristo, tumepata dhamiri safi. (Ebr. 10:19-23, 35, 36; Ufu. 7:9, 10, 14) Mtume Paulo aliwahimiza Wakristo wafanye mambo yote kwa utukufu wa Mungu ili wasiwakwaze wengine. Pia, mtume Petro alionyesha kwamba mwenendo mzuri wa Kikristo unaweza kuwavuta wasioamini waikubali kweli. (1 Kor. 10:31, 33; 1 Pet. 3:1) Unawezaje kumsaidia mtu astahili kuwa mhudumu wa habari njema?

      WAHUBIRI WAPYA

      5 Mara tu unapoanza kuongoza funzo la Biblia na mtu anayependezwa, mtie moyo awaambie wengine mambo anayojifunza. Anaweza kuwahubiria isivyo rasmi watu wa ukoo, marafiki, wafanyakazi wenzake, na watu wengine.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki