-
Makusanyiko ya Wilaya—Kipindi cha Ibada Chenye ShangweHuduma ya Ufalme—2010 | Juni
-
-
6. Tunapaswa kukumbuka nini kuhusu mavazi na mapambo yetu?
6 Mavazi na Mapambo: Wafanyabiashara wasio Wayahudi wangeweza kuitambua kwa urahisi familia ya Yesu na waabudu wengine Wayahudi waliokuwa wakisafiri kwenda na kurudi kutoka kwenye sherehe, kwa sababu miisho ya nguo zao ilikuwa na upindo wenye nyuzinyuzi, ambao ulikuwa na uzi wa bluu juu yake. (Hes. 15:37-41) Ingawa Wakristo hawavai mavazi fulani rasmi, tunajulikana kwa kuvaa mavazi yenye kiasi, nadhifu, na safi. Tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu mavazi na mapambo yetu tunaposafiri kwenda na kutoka kusanyikoni, na tunapokuwa kwenye jiji la kusanyiko. Hata tukibadili mavazi baada ya programu, tunapaswa kuvalia kwa njia inayomletea Yehova heshima na kuvaa beji yetu ya kusanyiko. Kwa njia hiyo, tutaonekana tofauti na watu wasio Mashahidi na sura yetu itakuwa yenye kuvutia.
-
-
Makusanyiko ya Wilaya—Kipindi cha Ibada Chenye ShangweHuduma ya Ufalme—2010 | Juni
-
-
◼ Viatu: Kila mwaka watu kadhaa hujeruhiwa kwa sababu ya viatu. Kwa hiyo, ni vizuri kuvaa viatu vya kawaida, vinavyokutoshea vizuri na vinavyokuwezesha kutembea kwenye ngazi, viunzi vya chuma, na maeneo mengine, bila kujikwaa.
-