Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Guyana
    2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Miaka minne baadaye, Evander J. Coward alifika Guyana na kutoa hotuba za Biblia kwa maelfu ya watu waliokusanyika kwenye kumbi za mji wa Georgetown na New Amsterdam.

      Frederick, mwana wa Phillip, anakumbuka ziara ya Coward. Anaandika: “Baada ya muda mfupi, Ndugu Coward alijulikana sana mjini Georgetown, na kwa sababu ya mahubiri yake, watu wenye kupendezwa walianza kujiunga na kikundi chetu cha Wanafunzi wa Biblia. Wakati huo tulijifunza kitabu kuhusu kusudi la Mungu (The Divine Plan of the Ages), kitabu kuhusu uumbaji mpya (The New Creation), na vitabu vinginevyo.

  • Guyana
    2005 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Katika barua aliyoandikia vyombo vya habari, Coward alieleza hali ya ulimwengu kwa kuilinganisha na unabii wa Biblia. Na kwenye ukumbi wa mji wa Georgetown, alitoa hotuba yenye kuchochea sana yenye kichwa “Kubomoa Kuta za Babiloni.”

      Ripoti moja katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Oktoba 1, 1983 inasema: “Makasisi walikasirika sana hivi kwamba waliwashawishi wenye mamlaka wamfukuze Ndugu Coward na kupiga marufuku vichapo kadhaa. Marufuku hiyo haikuondolewa hadi mwaka wa 1922.” Hata hivyo, watu wengi walimheshimu Coward kwa kuwa alihubiri kwa ujasiri. Hata alipokuwa akiondoka, walisimama gatini na kupaaza sauti: “Yeye tu ndiye aliyehubiri kweli.” Wafanyakazi wa bandari hata walitisha kugoma ili kupinga kufukuzwa kwa Coward, lakini ndugu wakawashauri wasifanye hivyo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki