-
Kupatanisha Sayansi na DiniAmkeni!—2002 | Juni 8
-
-
Kwa mfano, tunapoelewa kwamba Biblia hutumia usemi “siku” ili kuwakilisha vipindi mbalimbali vya wakati, basi tunaona kwamba simulizi la Mwanzo kuhusu siku sita za uumbaji halipingani na maelezo ya kisayansi yanayosema kwamba dunia imekuwapo kwa miaka bilioni nne na nusu hivi iliyopita. Kulingana na Biblia, dunia ilikuwapo kwa muda usiojulikana kabla ya siku za uumbaji kuanza. (Ona sanduku “Je, Kila Siku ya Uumbaji Ilikuwa na Saa 24 Tu?”) Hata wanasayansi wakirekebisha maelezo yao na kuonyesha kwamba dunia iliumbwa katika kipindi tofauti na hicho, bado maelezo ya Biblia ni ya kweli.
-
-
Kupatanisha Sayansi na DiniAmkeni!—2002 | Juni 8
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 10]
Je, Kila Siku ya Uumbaji Ilikuwa na Saa 24 Tu?
Watu fulani wenye imani kali ya kidini wanasema kwamba vitu vyote vinavyoonekana viliumbwa katika kipindi cha siku sita tu kati ya miaka 6,000 na 10,000 iliyopita, na kila siku ilikuwa na saa 24. Lakini kwa kufanya hivyo, wanaendeleza fundisho lisilopatana na Maandiko ambalo limewafanya watu wengi kuidharau Biblia.
Je, kila wakati ambapo Biblia inataja siku moja huwa inamaanisha kipindi cha saa 24? Mwanzo 2:4 inasema kuhusu “siku ile BWANA Mungu alipoziumba mbingu na nchi.” Siku hiyo moja inatia ndani siku zote sita za uumbaji zinazotajwa kwenye Mwanzo sura ya 1. Biblia hutumia neno siku kuonyesha kipindi cha wakati kilicho na urefu fulani na kinaweza kuwa cha miaka elfu moja au maelfu mengi ya miaka. Inawezekana kwamba kila siku ya uumbaji inayotajwa katika Biblia ilikuwa na maelfu ya miaka. Isitoshe, tayari dunia ilikuwepo hata kabla ya siku za uumbaji kuanza. (Mwanzo 1:1) Kwa hiyo, simulizi la Biblia linapatana na sayansi ya kweli katika jambo hilo.—2 Petro 3:8.
Akizungumzia kuhusu maoni ya kwamba siku za uumbaji zilikuwa saa 24 tu, mwanabiolojia wa molekuli Francis Collins anasema hivi: ‘Ile dhana ya kwamba kila siku ya uumbaji ilikuwa na saa 24 tu imepotosha sana imani ya watu wenye akili kuliko kitu kingine chochote hivi karibuni.’
-