Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sayansi na Kitabu cha Mwanzo
    Uhai—Ulitokana na Muumba?
    • Vipindi sita vya uumbaji

      Musa aliandika masimulizi yake katika Kiebrania, naye aliyaandika kwa njia inayopatana na maoni ya mtu aliye duniani. Mambo hayo mawili pamoja na ukweli wa kwamba ulimwengu ulikuwako kabla ya mwanzo wa vile vipindi au siku za uumbaji, yanasaidia kutatua ubishi mwingi kuhusu masimulizi ya uumbaji. Jinsi gani?

      Siku sita za uumbaji

      Matukio yaliyoanza “siku” moja yaliendelea katika “siku” ya pili au zaidi zilizofuata

      Kuchunguza kwa makini masimulizi ya kitabu cha Mwanzo kunafunua kwamba matukio yaliyoanza “siku” moja yaliendelea katika “siku” ya pili au zaidi zilizofuata. Kwa mfano, kabla ya “siku” ya kwanza ya uumbaji, mwanga wa jua, ambalo tayari lilikuwako, haukuwa ukifika duniani, labda kwa sababu ya mawingu mazito. (Ayubu 38:9) Katika “siku” ya kwanza, mawingu hayo yalianza kutanzuka na kuuruhusu mwanga upenye angani.a

      Katika “siku” ya pili, yaonekana kwamba anga lilizidi kutanzuka na kutokeza mgawanyiko kati ya mawingu mazito yaliyo juu na bahari. Katika “siku” ya nne, anga lilikuwa limetanzuka vya kutosha hivi kwamba jua na mwezi vingeweza kuonekana “katika anga la mbingu.” (Mwanzo 1:14-16) Yaani, kwa mtu aliye duniani, jua na mwezi vilianza kuonekana. Yote hayo yalitukia hatua kwa hatua.

      Pia, kulingana na masimulizi ya Mwanzo, kadiri anga lilivyozidi kutanzuka, viumbe vinavyoruka​—kutia ndani wadudu na viumbe vingine vyenye mabawa​—vilianza kuonekana katika “siku” ya tano.

      Kutokana na masimulizi ya Biblia, inawezekana kwamba matukio fulani muhimu ya kila siku, au kipindi cha uumbaji, hayakutendeka mara moja bali hatua kwa hatua, huenda hata baadhi ya matukio hayo yaliendelea hadi “siku” ya uumbaji iliyofuata.b

  • Sayansi na Kitabu cha Mwanzo
    Uhai—Ulitokana na Muumba?
    • b Kwa mfano, katika siku ya sita ya uumbaji, Mungu aliagiza kwamba wanadamu ‘wawe wengi waijaze dunia.’ (Mwanzo 1:28, 31) Hata hivyo, hilo lilianza kutimia katika “siku” inayofuata.​—Mwanzo 2:2.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki