-
Imani Yajaribiwa Huko SlovakiaAmkeni!—2002 | Desemba 22
-
-
Halafu, mnamo mwaka wa 1924, nikiwa na umri wa miaka 13, nilimwomba anibatize. Ingawa Mama aliniona kuwa mchanga sana kuchukua hatua hiyo nzito, nilimsadikisha kwamba huo ulikuwa uamuzi wangu thabiti. Hivyo, katika kusanyiko la siku moja lililofanywa katika mwezi wa Julai karibu na Mto Ondava, nilibatizwa katika maji ya mto huo ili kuonyesha wakfu wangu kwa Yehova.
-
-
Imani Yajaribiwa Huko SlovakiaAmkeni!—2002 | Desemba 22
-
-
Katika miaka ya 1930, nilipendelewa kuwa mjumbe kwenye makusanyiko makubwa kwenye jiji kuu la Prague. Katika mwaka wa 1932, kusanyiko la kwanza la kimataifa lilipangwa nchini Czechoslovakia. Tulikutana katika Jumba la Michezo ya Kuigiza la Varieté. Kichwa cha hotuba ya watu wote, “Ulaya Kabla ya Uharibifu,” kiliwavutia wengi, na karibu watu 1,500 walihudhuria. Kusanyiko jingine la kimataifa lilifanywa Prague mnamo mwaka wa 1937, na nilikuwa na pendeleo la kutoa hotuba moja. Wajumbe kutoka nchi nyingi za Ulaya walihudhuria, na sote tulitiwa moyo kuvumilia magumu yaliyofuata upesi wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu.
-
-
Imani Yajaribiwa Huko SlovakiaAmkeni!—2002 | Desemba 22
-
-
Baada ya vita, makusanyiko yalitupatia nguvu mpya ya kuendelea na kazi yetu. Mnamo Septemba 1946 kusanyiko la kwanza la nchi nzima lilifanywa katika jiji la Brno. Nilipendelewa kutoa hotuba yenye kichwa “Mavuno, Mwisho wa Ulimwengu.”
Mnamo mwaka wa 1947 kusanyiko jingine la kitaifa lilifanywa huko Brno. Wakati huo, Nathan H. Knorr, Milton G. Henschel, na Hayden C. Covington, waliozuru kutoka makao makuu ya ulimwengu ya Mashahidi wa Yehova huko Brooklyn, New York, walitoa hotuba zenye kutia moyo. Nilipendelewa kutafsiri hotuba zao. Ijapokuwa tulikuwa wahubiri 1,400 hivi wa Ufalme huko Czechoslovakia wakati huo, karibu watu 2,300 walihudhuria hotuba ya watu wote.
-