Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Tumegawanywa na Lugha Lakini Tumeunganishwa na Upendo”
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 1
    • Huko Prague mwanamume mmoja alikuwa akikaa katika mojawapo ya hoteli ambamo wajumbe wa kusanyiko waliotoka Uingereza walikuwa wakikaa. Jioni moja aliwaambia wajumbe hao kwamba yeye pia alihudhuria kusanyiko siku hiyo. Ni nini kilichomsukuma aende kusanyikoni? Mwanamume huyo alisema kwamba alilazimika kwenda kusanyikoni baada ya kupokea mialiko kutoka kwa wahubiri kumi tofauti-tofauti mitaani! Alivutiwa sana na alikuwa na hamu ya kujifunza mengi zaidi.—1 Timotheo 2:3, 4.

  • “Tumegawanywa na Lugha Lakini Tumeunganishwa na Upendo”
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 1
    • Wahudhuriaji wengi watakumbuka kusanyiko hilo kwa sababu nyingine. Kristina, dada Mcheki ambaye alijitolea kwenda pamoja na kikundi cha wajumbe kutoka ng’ambo waliosafiri kwa basi, anakumbuka hivi: “Tulipokuwa tukiagana, dada mmoja alinivuta kando, akanikumbatia na kusema: ‘Nilijisikia nimetunzwa vizuri sana! Ulituletea chakula kwenye viti vyetu na hata kutupa maji ya kunywa. Nakushukuru sana kwa upendo wako wa kujidhabihu.’” Alikuwa akizungumzia mpango wa chakula cha mchana kwa ajili ya wajumbe kutoka ng’ambo. Ndugu mmoja alieleza hivi: “Ilikuwa kazi ambayo hatukuwa tumewahi kufanya. Kazi hiyo ilihusisha kupeleka vifurushi 6,500 hivi vya chakula cha mchana kila siku. Tuliguswa moyo kuona wengi, kutia ndani watoto, wakijitolea kusaidia.”

  • “Tumegawanywa na Lugha Lakini Tumeunganishwa na Upendo”
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 1
    • Ndugu aliyefanya kazi katika Idara ya Upashaji wa Habari katika kusanyiko la Prague anasema: “Jumapili asubuhi (Siku ya Yenga), ofisa aliyewasimamia polisi waliotumwa kwenye kusanyiko alitutembelea. Aliona amani imetanda na akasema hawakuwa na kazi ya kufanya. Pia, alisema watu fulani wanaoishi karibu na uwanja huo walikuwa wameuliza kuhusu programu. Ofisa huyo alipotaja Mashahidi wa Yehova, kwa kawaida watu hao waliudhika, naye akawaambia: ‘Iwapo watu wangejiendesha kwa kadiri fulani kama Mashahidi wa Yehova, polisi hawangehitajiwa tena kamwe.’”

  • “Tumegawanywa na Lugha Lakini Tumeunganishwa na Upendo”
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 1
    • Katika kusanyiko la Prague hotuba zote zilitolewa katika Kicheki, Kiingereza, na Kirusi.

  • “Tumegawanywa na Lugha Lakini Tumeunganishwa na Upendo”
    Mnara wa Mlinzi—2007 | Julai 1
    • huko Prague, mji mkuu wa Jamhuri ya Cheki;

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki