-
Ni Nani Wanaoishi Katika Makao ya Roho?Amkeni!—1996 | Novemba 22
-
-
Mamilioni ya watu katika Afrika na kwingineko huamini kwamba kifo si mwisho wa uhai bali ni mgeuko tu, au kupita kuelekea uhai katika makao ya roho, mahali wanapokaa miungu na vilevile wazazi wa kale. Msomi John Mbiti, mtaalamu wa dini za Kiafrika, aandika juu ya itikadi katika wazazi wa kale, ambao awaita “wafu-wanaoishi”: “Hawa ndio ‘roho’ ambazo watu wa Afrika wanahangaikia . . . Wao wanajua na wana upendezi katika kile kinachoendelea katika familia zao [duniani]. . . . Wao ndio watunzaji wa mambo ya familia, mapokeo, maadili na utendaji wa familia. Makosa katika mambo haya kimsingi ni makosa dhidi ya mababu wa kale ambao, katika kiwango hicho, hutenda wakiwa viongozi wasioonekana wa familia na jumuiya. Kwa kuwa bado wanaonwa kuwa ‘watu,’ kwa hiyo wafu-wanaoishi ndio kikundi bora zaidi cha wapatanishi kati ya wanadamu na Mungu: wao wanajua mahitaji ya wanadamu, ‘majuzi’ walikuwa hapa pamoja na wanadamu, na kwa wakati huohuo wanaweza kufikia kikamili njia za kuwasiliana na Mungu.”
Ingawa hivyo, Biblia husema nini kuhusu hali ya wafu? Hiyo huonyesha kwamba hakuna kitu kama “wafu-wanaoishi.” Watu ama wako hai ama wamekufa—hawawezi kuwa katika hali zote mbili. Neno la Mungu hufundisha kwamba wafu hawawezi kusikia, kuona, kusema, au kufikiri. Wafu hawako katika hali yoyote ya kuweza kuongoza walio hai. Biblia husema: “Wafu hawajui neno lo lote . . . Mapenzi yao na machukio yao, na husuda yao, imepotea yote pamoja . . . Hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu [kaburini], uendako wewe.” (Mhubiri 9:5, 6, 10) “[Mwanadamu] huurudia udongo wake; siku hiyo mawazo yake yapotea.”—Zaburi 146:4.
Kurudi Mavumbini
Ikiwa waona hilo likiwa gumu kukubali, fikiria kile kilichompata mwanadamu wa kwanza, Adamu. Yehova alimfanya Adamu “kwa mavumbi ya ardhi.” (Mwanzo 2:7) Wakati Adamu alipokosa kutii amri ya Yehova, adhabu ilikuwa kifo. Mungu alimwambia: ‘Utairudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.’—Mwanzo 3:19.
Kabla ya Yehova kumuumba Adamu kutoka mavumbi, Adamu hakuwapo. Kwa hiyo wakati ‘aliporudi ardhini,’ akawa tena bila uhai, kama mavumbi. Yeye hakuvuka kuingia katika makao ya roho za wazazi wa kale. Yeye hakuenda mbinguni au helo. Alipokufa, huo ndio ulikuwa mwisho wake.
Je, jambo lilo hilo hupata wanadamu wengine wakati wa kifo? Ndivyo. Biblia hutaarifu: “Wote [wanadamu na wanyama] huendea mahali pamoja. Wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini hurudi tena.” (Mhubiri 3:20) Biblia huahidi kwamba Mungu atawaamsha wanadamu waliokufa warudi kwenye uhai katika dunia iliyo paradiso, lakini wakati huo bado utakuja. (Yohana 5:28, 29; Matendo 24:15) Kwa wakati uliopo, hatupaswi kuhofu wafu au kuwatolea dhabihu, kwa kuwa hawawezi kutusaidia wala kutudhuru.
Shetani na roho waovu wake wanataka kuongoza watu vibaya kuhusu hali ya wazazi wa kale waliokufa, kwa hiyo wanaendeleza uwongo kwamba watu huishi baada ya kifo. Njia moja wanayofanya hivyo ni kupitia hadithi zisizo za kweli. (1 Timotheo 4:1) Wao pia hutumia maono, ndoto, na wawasiliani-roho ili kudanganya watu wafikiri kwamba wamewasiliana na waliokufa. Lakini watu hawawasiliani na waliokufa. Badala ya hivyo, ni roho waovu ambao hujidai kuwa watu ambao wamekufa. Hiyo ndiyo sababu Yehova hushutumu sana wale wanaoulizia habari kutoka kwa wafu, ama moja kwa moja ama kwa njia isiyo ya moja kwa moja, kupitia njia nyinginezo, kama vile uaguzi.—Kumbukumbu la Torati 18:10-12.
-
-
Rafiki Yetu Bora Zaidi Yuko Katika Makao ya RohoAmkeni!—1996 | Novemba 22
-
-
Kwa kuwa wafu hawana uhai, hakuna faida yoyote iwezayo kupatikana kwa kuwaabudu. Kuwatolea wafu dhabihu huendeleza tu uwongo wa Shetani na roho waovu.
Je, malaika wa Mungu wanatamani tuwaabudu? Sivyo hata kidogo! Malaika waaminifu humpa Mungu utukufu na kuwatia moyo wanadamu wafanye vivyo hivyo. Mara mbili, Yohana alijaribu kuabudu malaika, lakini walimkemea, wakisema: “Angalia, usifanye hivi. . . . Msujudie Mungu.”—Ufunuo 19:10; 22:8, 9.
Shetani na roho waovu wake, tofauti na malaika waaminifu, hutaka waabudiwe na kupewa utukufu. Hili lilikuwa wazi wakati Shetani alipomjaribu Yesu akiwa mwanadamu duniani. Biblia husimulia: “Ibilisi akamchukua [Yesu] mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.”—Mathayo 4:8, 9.
Yesu alijibu: “Nenda zako, Shetani; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.” (Mathayo 4:10) Yesu alijua Sheria ya Yehova, naye akakataa kuivunja.—Kumbukumbu la Torati 6:13.
Ingawa Shetani hakuweza kumfanya Yesu amwabudu, amefaulu na wengine. Bila shaka, ni watu wachache wanaomwabudu Shetani kwa kutaka kwao wenyewe. Hata hivyo, kwa njia ya werevu, hila, uwongo, na hofu, Shetani na roho waovu wamepotosha watu wengi sana kutoka kwa ibada ya Yehova hivi kwamba mtume Yohana akaandika: “Dunia yote pia hukaa katika yule mwovu.” (1 Yohana 5:19) Wale wanaoabudu katika njia zilizo kinyume cha Neno la Mungu humheshimu Shetani, si Yehova. Biblia huonya: “Vitu vile wavitoavyo sadaka wavitoa kwa mashetani, wala si kwa Mungu.”—1 Wakorintho 10:20.
-