-
Kufaidika na Ushikamanifu wa Wapendwa WanguMnara wa Mlinzi—2006 | Septemba 1
-
-
Kufikia wakati huo, John alikuwa na ugonjwa ambao ulitutia wasiwasi. Katika 1948 aliugua kifua kikuu, naye alikuwa dhaifu mara nyingi. Alikuwa na dalili kama za mafua na ilimbidi alale mara nyingi, naye hangeweza kufanya chochote wala kumwona yeyote. Daktari tuliyemwomba mashauri kabla ya kualikwa kwenye ofisi ya tawi alisema kwamba John ameshuka moyo.
-
-
Kufaidika na Ushikamanifu wa Wapendwa WanguMnara wa Mlinzi—2006 | Septemba 1
-
-
Kukabiliana na Ugonjwa wa John
Kufikia miaka ya 1970, ilikuwa wazi kwamba afya ya John iliendelea kuwa mbaya. Hatua kwa hatua, ilibidi aache baadhi ya mapendeleo yake ya utumishi, kutia ndani kuongoza funzo la Mnara wa Mlinzi la kila juma na mazungumzo ya Biblia ya asubuhi kwenye ofisi ya tawi. Alipelekwa kwenye Idara ya Utumishi, kisha katika ofisi ya barua, halafu kwenye bustani.
Kwa kuwa John hakukata tamaa kwa urahisi, ilikuwa vigumu kwake kufanya mabadiliko. Niliposisitiza kwamba anahitaji kupumzika, alisema kwa mzaha kwamba mimi ni kizuizi kwake, kisha akanikumbatia kwa upendo. Hatimaye tuliona ni afadhali tutoke katika eneo la Kireno na kutumikia katika kutaniko lililokutana kwenye Jumba la Ufalme la ofisi ya tawi.
Afya ya John ilipoendelea kuzorota, nilitiwa moyo kuona akiwa na uhusiano wa karibu pamoja na Yehova. Wakati John alipoamka katikati ya usiku akiwa ameshuka moyo sana, tulizungumza pamoja mpaka alipotulia na tukasali ili kumwomba Yehova msaada. Hatimaye, aliweza kukabiliana na hali hizo mbaya akiwa peke yake kwa kujilazimisha kukariri polepole maneno haya ya Wafilipi 4:6, 7: “Msihangaike juu ya kitu chochote . . .” Kisha angetulia kiasi cha kuweza kusali. Mara nyingi nilikuwa macho na ningetazama akifungua mdomo wake huku akimsihi Yehova kwa unyoofu.
-