Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uhodari Waimarishwa kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 1
    • Fikiria mfano wa Namangolwa aliyelelewa katika familia ya Kikristo huko Zambia. Alipokuwa na umri wa miaka miwili, Namangolwa alilemaa. Anasema hivi: “Nilikuwa nikijifikiria sana, nikifikiri kwamba watu watashtuliwa na umbo langu. Lakini ndugu zangu wa kiroho walinisaidia kuona mambo kwa njia tofauti. Kwa hiyo, niliacha kujifikiria sana, na baada ya muda nikabatizwa.”

      16 Ingawa Namangolwa ana kiti cha magurudumu, mara nyingi yeye hulazimika kutembea kwa mikono na magoti anapokuwa kwenye barabara ya mchanga. Hata hivyo, yeye hufanya upainia msaidizi angalau miezi miwili kila mwaka. Mwenye nyumba mmoja alilia wakati Namangolwa alipomhubiria. Kwa nini? Kwa sababu alichochewa sana na imani na uhodari wa dada yetu. Yehova amembariki sana Namangolwa kwa kuwa watano kati ya wanafunzi wake wa Biblia wamebatizwa, na mmoja ni mzee wa kutaniko. Namangolwa anasema hivi: “Mara nyingi miguu yangu huniuma sana, lakini siachi jambo hilo linizuie.” Dada huyo ni mmoja wa Mashahidi wengi ulimwenguni walio dhaifu kimwili lakini wenye bidii nyingi kwa sababu wanampenda Mungu na jirani. Watu kama hao ni wenye kutamanika sana machoni pa Yehova!—Hagai 2:7.

  • Uhodari Waimarishwa kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Oktoba 1
    • [Picha katika ukurasa wa 24]

      Namangolwa Sututu

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki