-
Kuchunguza Chembe kwa HadubiniAmkeni!—1999 | Septemba 8
-
-
(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)
Jinsi Protini Zinavyofanyizwa
Ili ieleweke kwa urahisi, tunatoa kielezi cha protini ambayo imefanyizwa kwa asidi-amino 10. Protini nyingi zina zaidi ya amino asidi 100
1 Protini ya pekee hufunua sehemu ya nyuzi za DNA
Protini
2 Misingi huru ya RNA huungana na misingi iliyo wazi ya DNA kwenye uzi mmoja peke yake, na hilo hutokeza uzi wa RNA unaopeleka ujumbe
Misingi huru ya RNA
3 RNA yenye kupeleka ujumbe ambayo imetoka kufanyizwa huachana na DNA na kuelekea kwenye ribosomu
4 RNA ya kuhamisha hubeba asidi-amino moja na kuipeleka kwenye ribosomu
RNA inayohamisha
Ribosomu
5 Mnyororo wa asidi-amino huunganishwa pamoja wakati ribosomu inapopitia RNA inayopeleka ujumbe
Asidi-amino
6 Mnyororo wa protini unaofanyizwa huanza kujikunja katika umbo linalofaa ili kutekeleza kazi inavyofaa. Kisha mnyororo huo huachiliwa na ribosomu
RNA ya kuhamisha ina sehemu mbili muhimu:
Sehemu moja hutambua uzi wa RNA unaopeleka ujumbe
Sehemu nyingine hubeba asidi-amino inayofaa
RNA ya kuhamisha
Misingi ya RNA hutumia U badala ya T, kwa hiyo U huungana na A
A U Uracil
U A Adenine
-
-
Uhai Ulianzaje?Amkeni!—1999 | Septemba 8
-
-
Uhai Ulianzaje?
MOLEKULI ya DNA hutekeleza mambo ya kustaajabisha. DNA hutimiza mambo mawili yanayohitajiwa na chembe zako katika kufanyiza visehemu vya urithi. Kwanza, DNA hunakiliwa sawasawa ili habari iweze kupitishwa kutoka kwa chembe moja hadi nyingine. Pili, mfuatano wa DNA husaidia chembe kujua aina ya protini itakayofanyiza, na hivyo kuamua chembe hiyo itakuwa ya aina gani na kazi itakayofanya. Hata hivyo, DNA haitekelezi kazi hizi bila msaada. Protini nyingi za kipekee huhusika.
DNA peke yake haiwezi kutokeza uhai. Ina maagizo yote yanayohitajiwa ili kufanyiza protini zote zinazohitajiwa na chembe hai, kutia ndani zile zinazonakili DNA kwa ajili ya kizazi kingine cha chembe na zile zinazosaidia DNA kufanyiza protini mpya. Ingawa hivyo, habari chungu nzima iliyohifadhiwa katika chembe za urithi za DNA ni bure pasipo RNA na protini za kipekee, zinazotia ndani ribosomu, zinazohitajiwa ili “kusoma” na kutumia habari hiyo.
Wala protini peke yake haziwezi hutokeza uhai. Protini iliyo peke yake haiwezi kutokeza chembe ya urithi iliyo na maagizo ya kufanyiza protini za aina ileile.
Kwa hiyo, kufumbua fumbo la uhai kumeonyesha nini? Elimu ya kisasa ya chembe za urithi na biolojia ya molekuli imetoa uthibitisho wa kutosha wa uhusiano ulio tata sana wenye kutegemeana kati ya DNA, RNA, na protini. Matokeo haya yanaonyesha kwamba uhai hutegemea kuwapo kwa elementi hizi zote kwa wakati mmoja. Hivyo, uhai haungeweza kamwe kutokea tu ghafula kwa nasibu.
-