-
Mapendekezo ya Kutoa BroshuaHuduma ya Ufalme—2005 | Julai
-
-
Mapendekezo ya Kutoa—Je! Kweli Mungu Anatujali?
Baada ya kutaja msiba fulani uliotokea, unaweza kusema:
“Umewahi kujiuliza kwa nini Mungu huwaacha wanadamu wateseke ikiwa kweli anatujali? [Mruhusu ajibu.] Broshua hii inajibu swali hilo vizuri na inaonyesha mambo ambayo Mungu atafanya hivi karibuni. [Mwonyeshe picha kwenye ukurasa wa 27, kisha usome Zaburi 145:16 katika fungu la 22.] Mungu atakomeshaje mateso yote yanayowakumba wanadamu? Ningependa kuzungumzia swali hilo nitakaporudi.” Mtolee broshua, na upange kurudi.
-
-
Mapendekezo ya Kutoa BroshuaHuduma ya Ufalme—2005 | Julai
-
-
Mhubiri kijana anaweza kusema:
“Vijana wengi wa rika langu wanajiuliza jinsi ulimwengu utakavyokuwa miaka 10 au 15 ijayo. Unafikiri ulimwengu utakuwaje wakati huo? [Mruhusu ajibu.] Matatizo tunayoona leo yanaonyesha kwamba tunaishi katika siku za mwisho. [Soma 2 Timotheo 3:1-3.] Broshua hii inajibu maswali haya. [Soma maswali yaliyo kwenye jalada, kisha umtolee broshua.] Ningependa kurudi, ikiwa utakuwa na dakika chache, ili nikuonyeshe habari fulani yenye kutia moyo kuhusu mwisho wa magonjwa na kuzeeka.” Fanya mpango wa kurudi.
-
-
Mapendekezo ya Kutoa BroshuaHuduma ya Ufalme—2005 | Julai
-
-
Mtu mzima anapohubiri na mtoto, anaweza kujitambulisha pamoja na mtoto huyo na kusema:
“Ukimruhusu, ________ angependa kukusomea andiko moja. [Mtoto anasoma Zaburi 37:29 na kutoa maelezo mafupi.] Broshua hii inazungumzia jinsi Mungu atakavyotimiza kusudi lake kuelekea wanadamu na dunia. [Mwonyeshe picha kwenye ukurasa wa 24-27.] Tutakaporudi, nitakuonyesha ahadi nzuri sana ya Biblia kuhusu ufufuo.” Mtolee broshua, na upange kumrudia.
-