-
Uzuri Mwingi Mno wa Kiti cha Ufalme cha Yehova cha KimbinguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Yeye aandika hivi: “Baada ya vitu hivi mimi nikaona, na, tazama! mlango uliofunguliwa katika mbingu, na sauti ya kwanza ambayo mimi nilisikia ilikuwa kama ya tarumbeta, ikinena na mimi, ikisema: ‘Njoo juu huku, na mimi nitaonyesha wewe vitu ambavyo ni lazima vitukie.’” (Ufunuo 4:1, NW) Yohana katika njozi anapenya zile mbingu zisizoonekana za kuwapo kwa Yehova, mwenye kukwezwa juu sana zaidi ya anga za juu zaidi kama zinavyovumbuliwa na wanaanga, hata juu zaidi ya magalaksi ya ulimwengu wote mzima wa kimwili. Kana kwamba kwa kuingia mlango uliofunguliwa, Yohana anaalikwa alishe macho yake karamu ya mandhari nzuri sana ya kustaajabisha ya mbingu za kiroho zilizo za mwisho kabisa kabisa ambako Yehova mwenyewe anakalia kiti cha ufalme. (Zaburi 11:4; Isaya 66:1)
-
-
Uzuri Mwingi Mno wa Kiti cha Ufalme cha Yehova cha KimbinguUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
Bila shaka, Yehova ndiye Chanzo adhimu cha mialiko hiyo. (Ufunuo 1:1) Yeye amefungua mlango ili Yohana, katika njozi, aweze kuingia mahali patakatifu zaidi sana katika milki yote iliyo kubwa mno ya enzi kuu ya Yehova.
-