Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yusufu Anawekwa Katika Gereza
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
    • Baadaye Farao akamkasirikia mnyweshaji wake na mwokaji wake, na kuwatia gerezani. Usiku mmoja kila mmoja wao anaota ndoto ya pekee, lakini hawajui maana ya ndoto zao, kesho yake Yusufu anasema: ‘Niambieni ndoto zenu.’ Wanamwambia. Na kwa msaada wa Mungu, Yusufu anawaambia maana ya ndoto zao.

      Kwa mnyweshaji, Yusufu anasema: Kwa siku tatu utafunguliwa utoke gerezani , uwe mnyweshaji wa Farao tena.’ Lakini kwa mwokaji, Yusufu anasema: ‘Katika siku tatu Farao atakukata kichwa chako.’

      Katika muda wa siku tatu inakuwa kama Yusufu alivyosema. Farao anamkata kichwa mwokaji wake. Lakini mnyweshaji, anafunguliwa gerezani na kuanza kumtumikia mfalme tena. Lakini mnyweshaji huyo anamsahau Yusufu! Hamwambii Farao habari zake, naye Yusufu anaendelea kukaa gerezani.

  • Ndoto za Farao
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
    • Farao akiota ndoto

      HADITHI YA 23

      Ndoto za Farao

      MIAKA miwili inapita, Yusufu angali gerezani. Mnyweshaji hamkumbuki. Ndipo usiku mmoja Farao anaota ndoto mbili za pekee sana, naye hajui maana yazo. Unamwona akilala pale? Kesho yake Farao anawaita wenye akili na kuwaambia mambo ambayo ameota. Lakini hawawezi kumwambia maana ya ndoto zake.

      Mwishowe yule mnyweshaji anakumbuka Yusufu. Anamwambia Farao hivi: ‘Nilipokuwa gerezani alikuwako mtu huko aliyeweza kuniambia maana ya ndoto.’ Farao anaagiza Yusufu atolewe gerezani mara moja.

      Farao anamsimulia Yusufu ndoto zake hivi: ‘Niliona ng’ombe saba wanono na wazuri. Kisha nikawaona ng’ombe saba waliokonda sana. Na wale waliokonda wakawala ng’ombe wanono.’

      Ng’ombe saba wanono, ng’ombe saba waliokonda

      ‘Katika ndoto yangu ya pili niliona masuke saba yenye kujaa nafaka zilizoiva, yakikua katika bua moja. Kisha nikaona masuke saba membamba, yaliyokauka sana ya nafaka. Na yale masuke membamba ya nafaka yalianza kumeza masuke mazuri saba ya nafaka.

      Yusufu anamwambia Farao hivi: ‘Maana ya ndoto zile mbili ni moja. Wale ng’ombe saba wanono na masuke saba ya nafaka yenye kujaa ni miaka saba, na wale ng’ombe saba waliokonda na masuke ya nafaka membamba saba ni miaka mingine saba. Kutakuwako miaka saba ya chakula kingi katika Misri. Kisha itakuwako miaka saba ya chakula kidogo sana.’

      Masuke saba membamba yaliyokauka sana ya nafaka, masuke saba yenye kujaa nafaka zilizoiva

      Basi Yusufu anamwambia Farao hivi: ‘Mchague mtu mwenye akili awe msimamizi wa kukusanya chakula wakati wa miaka mizuri saba. Hapo watu hawatakufa njaa wakati wa miaka mibaya saba inayofuata ya chakula kidogo.’

      Farao anapenda wazo hilo. Anamchagua Yusufu akusanye chakula, na kukiweka akiba. Yusufu anakuwa mkuu katika misri, wa pili kwa Farao.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki