Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Brolga, Kasowari, Emu, na Jabiru—Baadhi ya Ndege Wenye Kutazamisha wa Australia
    Amkeni!—1996 | Novemba 8
    • Tai Mwenye Mkia Wenye Umbo la Kabari—Mfalme wa Anga

      Umbali mfupi kutoka kilele chenye miamba cha mlima fulani katika Victoria, na kukabili upepo mwingi wenye nguvu ambao ulifukuza ndege wale wengine wote kutoka angani, tai mwenye mkia wenye umbo la kabari alikuwa akicheza hewani. Mwandikaji David Hollands alishuhudia wonyesho wa ustadi wa michezo ya hewani ambao huenda hangepata kuuona kamwe: “Tai huyo alijiangika juu kule,” yeye aandika, “bila kusonga na akiwa starehe kabisa katika mahali hapo penye msukosuko. . . . Nilipokuwa nikitazama, aliruka chini, akifumba mabawa yake ili ajitose wima. Aliteremka kwa meta mia moja kisha mabawa yakafunuka kidogo sana, hilo likimrusha kuelekea juu ili kufikia kimo ambacho alikuwa amepoteza wakati wa kuruka chini. . . . Alijisawazisha kwa kubiringika nusu, kisha akapuruka juu zaidi [na] kurudia mruko wa chini tena na tena, akipita mbio sana kwa kutazamisha kuingia kwenye sakafu ya bonde na kupanda juu tena katika wonyesho uliodumishwa wenye kufurahisha.”

      Akiwa na upana wa mabawa wa meta 2.5 na mkia wenye umbo la kabari, haiwezekani kukosa kumtofautisha mfalme huyo mwenye madaha na nguvu na ndege mwingine yeyote katika anga za Australia. Kucha zake zaweza kubana kwa kani ya tani tatu! Hata hivyo, kwa kipindi fulani cha wakati, njia “ifaayo” tu ambayo watu walimwona tai mwenye mkia wenye umbo la kabari ilikuwa kupitia mtutu wa bunduki wakati walipomwinda. Sawa na binamu yake furukombe wa Marekani, ambaye alipigwa risasi bila huruma ili kulinda samaki aina ya salmoni na biashara za manyoya, tai huyu wa Australia alinyanyaswa kwa kuua kondoo mara kwa mara. “Ni ndege wengine wachache wawindaji ulimwenguni,” chasema kitabu Birds of Prey, “ambao wamenyanyaswa vibaya sana kama vile Tai mwenye mkia wenye umbo la Kabari . . . Kwa karibu miaka 100 alionwa kuwa mwindaji . . . , na fedha zililipwa kwa wale walioonyesha uthibitisho kwamba walimuua.”

      Hata hivyo, baada ya miaka mingi, mashtaka hayo yaliondolewa. Mlo wake mkuu ulithibitika kuwa sungura wa mwituni na pindi kwa pindi wanyama wenyeji, kutia ndani walabi walio na karibu uzito mara mbili wa uzito wa ndege huyo. Ufunuo huo, hatimaye, ulimpa tai huyo urafiki pamoja na mwanadamu na vilevile ulinzi wa kisheria.

  • Brolga, Kasowari, Emu, na Jabiru—Baadhi ya Ndege Wenye Kutazamisha wa Australia
    Amkeni!—1996 | Novemba 8
    • Tai

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki