-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Lakini dunia ikaja kusaidia mwanamke, na dunia ikafungua kinywa chayo na ikameza kabisa mto ambao yule drakoni alitapika kutoka kinywa chake.
-
-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Dunia”—elementi zilizo ndani ya mfumo wa mambo wa Shetani mwenyewe—ikaanza kumeza ule “mto,” au “furiko.” Wakati wa miaka ya 1940 Mashahidi walianza kupata mfululizo wa maamuzi yenye kupendeleka katika Mahakama Kuu Zaidi Sana ya United States, na kutoka mamlaka zenye kutawala katika mabara fulani, ambayo yalitetea uhuru wa ibada. Mwishowe, Mataifa-Mafungamani yakameza kabisa hiyo kani kubwa gandamizi ya Kinazi-Fashisti, kwa kuauni Mashahidi ambao walikuwa wameteseka chini ya tawala katili za kidikteta. Minyanyaso haikukoma kabisa, kwa kuwa yule drakoni ameendelea mpaka leo hii, naye huendeleza vita dhidi ya wale ambao “wana kazi ya kutoa ushahidi kwa Yesu.” Katika mabara mengi, Mashahidi washikamanifu wangali wamo gerezani, na baadhi yao wangali wanakufa kwa sababu ya ukamilifu wao. Lakini katika mengine ya mabara haya, wakati kwa wakati wenye mamlaka hulegeza mbano wao, na Mashahidi hufurahia kipimo kikubwa zaidi cha uhuru.c Hivyo, katika utimizo wa unabii, dunia huendelea kumeza mto wa mnyanyaso.
30. (a) Dunia imeandaa muawana wa kutosha kwa ajili ya kitu gani kitukie? (b) Ukamilifu wa watu wa Mungu hutokeza nini?
30 Katika njia hii, dunia imeandaa muawana wa kutosha kuruhusu kazi ya Mungu iendelee kwenye mabara 235 hivi na kuzaa wahubiri wa habari njema waaminifu zaidi ya milioni sita.
-
-
Ufalme wa Mungu Wazaliwa!Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
[Picha katika ukurasa wa 185]
“Dunia Ikafungua Kinywa Chayo”
Furiko-bubujiko la Shetani lenye mnyanyaso limefunguliwa katika mabara mengi dhidi ya Wakristo wapakwa-mafuta na waandamani wao. Hata hivyo, mara nyingi matukio katika mfumo wa mambo wa Shetani mwenyewe yametokeza kumezwa kabisa kwa furiko hilo.
Furiko la kughasiwa na kutiwa gerezani katika United States lilimezwa kabisa na maamuzi ya Mahakama Kuu Zaidi Sana yenye kupendeleka wakati wa miaka ya 1940.
1945: Mnyanyaso wenye ukatili katika mabara yaliyotawalwa na Ujeremani na Japani ulisimamishwa na ushindi wa Mataifa-Mafungamani katika Vita ya Ulimwengu 2.
Marufuku ilipowekwa juu ya Mashahidi wa Yehova katika Jamhuri ya Dominika, Mashahidi walitiwa gerezani, wakapigwa viboko, na wakapigwa kwa matako ya bunduki. Katika 1960 kutosikizana kati ya dikteta Rafael Trujilo na Kanisa Katoliki la Roma kuliongoza kwenye kuondolewa kwa marufuku juu ya Mashahidi wa Yehova.
Kupigwa risasi, kuchomwa moto, kulalwa kinguvu, kupigwa, kuteswa-teswa, na kuuawa kwa Mashahidi wakati wa vita ya wenyewe kwa wenyewe katika Naijeria kulikoma 1970 wakati majeshi ya serikali yaliposhinda mkoa wenye kujitenga ambako mambo hayo yalikuwa yakitukia.
Katika Hispania nyumba zilivamiwa na Wakristo wakafainiwa na kutiwa gerezani kwa ajili ya “uhalifu” wa kuongea juu ya Mungu na kufanya mikutano ya Kikristo. Mnyanyaso huu ulikoma mwishowe 1970, wakati kama tokeo la serikali kubadili sera yayo kuelekea dini zisizo za Kikatoliki, Mashahidi wa Yehova waliruhusiwa kuandikishwa kisheria.
Katika Ureno mamia ya nyumba yalipekuliwa bila waranti. Mashahidi waliumizwa kimwili na kutupwa gerezani, na wakanyang’anywa Biblia zao. Uvamizi-haramu huu ‘ulimezwa kabisa’ wakati, katika 1974, pinduzi la kijeshi lilipotokeza badiliko la serikali na sheria ikapitishwa ikitoa uhuru wa kukusanyika.
Katika Ajentina, chini ya serikali ya kijeshi, watoto wa Mashahidi wa Yehova walifukuzwa shuleni, na Mashahidi kuzunguka nchi wakakamatwa kwa kuhubiri habari njema. Mnyanyaso huu ulikoma mwishowe katika 1984 wakati serikali iliyokuwa ikitawala wakati huo ilipotambua kisheria Shirika la Mashahidi wa Yehova.
-