-
Yale Ambayo Siku ya Yehova ItafunuaMnara wa Mlinzi—2010 | Julai 15
-
-
4. “Dunia” ni nini, nayo itaharibiwa jinsi gani?
4 “Dunia” inafananisha ulimwengu wa wanadamu uliotengwa mbali na Mungu. Ulimwengu kama huo ulikuwepo katika siku za Noa, Mungu akaamuru uangamizwe kupitia Gharika. “Kwa neno hilohilo mbingu na dunia za sasa zimewekwa akiba kwa ajili ya moto nazo zinahifadhiwa mpaka ile siku ya hukumu na ya kuangamizwa kwa watu wasiomwogopa Mungu.” (2 Pet. 3:7) Ingawa Gharika iliwaangamiza watu wote wasiomwogopa Mungu kwa wakati mmoja, uharibifu unaokuja utatukia hatua kwa hatua wakati wa “ile dhiki kuu.” (Ufu. 7:14) Katika hatua ya kwanza ya dhiki hiyo, Mungu atawachochea viongozi wa kisiasa wa ulimwengu huu waharibu “Babiloni Mkubwa,” na hivyo kuonyesha kwamba amechukizwa na kahaba huyo wa kidini. (Ufu. 17:5, 16; 18:8) Kisha, katika vita vya Har–Magedoni, ambavyo vitakuwa hatua ya mwisho ya ile dhiki kuu, Yehova mwenyewe ataondolea mbali sehemu inayobaki ya ulimwengu wa Shetani.—Ufu. 16:14, 16; 19:19-21.
-
-
Yale Ambayo Siku ya Yehova ItafunuaMnara wa Mlinzi—2010 | Julai 15
-
-
“Dunia na Kazi Zilizo Ndani Yake Zitafunuliwa”
8. Dunia na kazi zake “zitafunuliwa” jinsi gani?
8 Petro alimaanisha nini alipoandika kwamba “dunia na kazi zilizo ndani yake zitafunuliwa”? Neno “zitafunuliwa” linaweza pia kutafsiriwa “zitafichuliwa” au “zitawekwa wazi.” Petro alimaanisha kwamba wakati wa ile dhiki kuu, Yehova atafunua wazi ulimwengu wa Shetani, na ataonyesha waziwazi kwamba unampinga Yeye na Ufalme Wake na hivyo unastahili kuharibiwa. Likizungumzia kwa njia ya unabii kuhusu wakati huo, andiko la Isaya 26:21 linasema hivi: “Yehova anakuja kutoka mahali pake ili kulitoza hesabu kosa la mkaaji wa nchi juu yake, na nchi hakika itafunua umwagaji wake wa damu wala haitawafunika tena watu wake waliouawa.”
9. (a) Tunapaswa kukataa nini, na kwa nini? (b) Tunapaswa kusitawisha sifa gani, na kwa nini?
9 Wakati wa siku ya Yehova, wale ambao wamefinyangwa na ulimwengu na roho yake mbovu wataonyesha jinsi walivyo kikweli, hata watachinjana wenyewe kwa wenyewe. Kwa kweli, inawezekana kwamba aina mbalimbali za burudani zenye jeuri ambazo zimeenea sana leo zinazoeza akili za wengi kwa ajili ya wakati ambapo mkono wa kila mtu “utainuka juu ya mkono wa mwenzake.” (Zek. 14:13) Hivyo basi, ni jambo la maana kama nini kwetu tuepuke kitu chochote kama vile sinema, vitabu, michezo ya video, na kadhalika, ambacho kinaweza kukuza ndani yetu tabia zinazomchukiza Mungu, kama vile kiburi na kupenda jeuri! (2 Sam. 22:28; Zab. 11:5) Badala yake, acheni tusitawishe sifa za tunda la roho takatifu ya Mungu, kwa kuwa sifa hizo zitastahimili joto kali la siku ya Yehova.—Gal. 5:22, 23.
-