-
Tetemeko la ArdhiAmkeni!—2002 | Machi 22
-
-
Ukubwa na Kiwango
Tetemeko la ardhi laweza kupimwa kulingana na ukubwa au kiwango chake. Katika miaka ya 1930, Charles Richter alibuni kipimo cha kuonyesha ukubwa wa matetemeko ya ardhi. Wakati vituo vya kupima matetemeko ya ardhi vilipoongezeka, vipimo vipya vilibuniwa kwa kutumia uvumbuzi wa Richter. Kwa mfano, kipimo cha nguvu za tetemeko la ardhi huonyesha kiasi cha nishati inayotokezwa kwenye chanzo cha tetemeko la ardhi.
Kwa wazi, nyakati nyingine vipimo hivyo havilingani na uharibifu uliosababishwa na tetemeko la ardhi. Kwa mfano, fikiria tetemeko la ardhi lililotokea kaskazini mwa Bolivia mnamo Juni 1994. Tetemeko hilo lilikuwa na ukubwa wa 8.2 kwenye kipimo cha Richter na yaripotiwa kwamba watu watano tu walikufa. Lakini, mamia ya maelfu ya watu walikufa katika tetemeko la ardhi lililotokea mwaka wa 1976 huko Tangshan, China, ambalo lilikuwa na ukubwa wa 8.0!
Tofauti na kipimo cha ukubwa, kiwango cha tetemeko la ardhi huonyesha jinsi linavyoathiri watu, majengo, na mazingira. Kiwango cha tetemeko la ardhi huonyesha waziwazi hasa jinsi wanadamu wanavyoathiriwa sana nalo. Kwa hakika, matetemeko hayawajeruhi watu moja kwa moja. Badala yake, majeraha na vifo husababishwa na kuta zinazoanguka, mabomba ya gesi yanayolipuka, nyaya za nguvu za umeme zinazokatika, vitu vinavyoporomoka, na kadhalika.
-
-
Tetemeko la ArdhiAmkeni!—2002 | Machi 22
-
-
a Kipima-tetemeko ni chombo kinachopima na kurekodi mtikisiko wa ardhi wakati tetemeko la ardhi linapotokea. Kipima-tetemeko cha kwanza kilibuniwa mwaka wa 1890. Siku hizi kuna vituo zaidi ya 4,000 ulimwenguni pote vinavyopima matetemeko ya ardhi.
-