Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sehemu ya 5—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Kisha, katika 1985 Mashahidi wa Yehova waliweza kufanya mikusanyiko minne mikubwa katika stediamu kubwa zaidi nchini Poland wakati wa mwezi wa Agosti. Wakati mjumbe kutoka Austria alipowasili kwa ndege, alishangaa kusikia tangazo kutoka kwa vikuza-sauti la kuwakaribisha Mashahidi wa Yehova nchini Poland kwa mkusanyiko wao. Akijua kwamba hilo lilionyesha kulikuwa na badiliko katika mtazamo wa serikali, Shahidi Mpoland mzee-mzee aliyekuwa hapo kuwakaribisha wageni hangeweza kujizuia kutokwa na machozi ya shangwe. Waliohudhuria mikusanyiko hiyo walikuwa wajumbe 94,134, kutia vikundi kutoka nchi 16. Je, umma ulijua kile kilichokuwa kikiendelea? Naam, ulijua! Wakati na baada ya mikusanyiko hiyo, walisoma ripoti katika magazeti yao makuu, wakaona umati wa mkusanyiko kwenye televisheni, na kusikia sehemu za programu kwenye redio zao. Wengi wao walipenda yale waliyoona na kusikia.

      Mipango kwa ajili ya mikusanyiko mikubwa hata zaidi katika Poland ilikuwa inaendelea, mnamo Mei 12, 1989, serikali ilipotoa utambulisho wa kisheria kwa Mashahidi wa Yehova kuwa shirika la kidini. Katika muda wa miezi mitatu, mikusanyiko mitatu ya kimataifa ilikuwa ikiendelea—katika Chorzów, Poznan, na Warsaw—kukiwa na jumla ya hudhurio la 166,518. Kwa kustaajabisha, maelfu ya Mashahidi kutoka zile nchi zilizokuwa Muungano wa Sovieti (U.S.S.R.) na Chekoslovakia waliweza kupata ruhusa iliyohitajiwa ya kusafiri na walihudhuria. Je, kazi ya kufanya wanafunzi ya Mashahidi wa Yehova ilikuwa inazaa matokeo katika nchi hizo ambako kutoamini kuwako kwa Mungu kulikuwa kumeungwa mkono sana na Serikali kwa miongo ya miaka? Jibu lilikuwa wazi wakati 6,093, kutia na vijana wengi, walipojitoa kwa ajili ya uzamisho wa maji kwenye mikusanyiko hiyo.

      Umma ungeweza kuona wazi sana kwamba Mashahidi walikuwa tofauti—kwa njia yenye kufaa sana. Kwenye magazeti ya umma, walisoma taarifa kama zile zifuatazo: “Wale wanaoabudu Yehova Mungu—kama vile wanavyosema wenyewe—huthamini sana vikusanyiko vyao, ambavyo kwa kweli ni udhihirisho wa umoja miongoni mwao. . . . Kuhusu utaratibu, hali ya amani, na usafi, washiriki wa mkusanyiko ni mifano ya kuigwa.” (Życie Warszawy)

  • Sehemu ya 5—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Hata kabla ya kutambuliwa kisheria, washiriki wa Baraza Linaloongoza walikuwa wamezuru hesabu fulani ya nchi kuona yale ambayo yangeweza kufanywa ili kusaidia ndugu zao Wakristo. Baada ya marufuku kuondolewa, walisafiri kwenye sehemu hizo nyingi ili kusaidia kupanga kazi. Katika muda wa miaka michache, walikuwa wamekutana binafsi na kuzungumza na Mashahidi nchini Poland, Hungaria, Rumania, Chekoslovakia, Urusi, Ukrainia, Estonia, na Belarus.

      Mikusanyiko ilipangwa ili kuimarisha Mashahidi wanaoishi katika nchi hizo na kujulisha sana umma kuhusu ujumbe wa Ufalme wa Mungu. Katika muda unaopungua miezi mitano baada ya marufuku kuondolewa na ile nchi iliyokuwa GDR wakati huo, mkusanyiko kama huo ulifanywa kwenye Stediamu ya Olympia ya Berlin. Mashahidi kutoka nchi nyinginezo 64 waliitikia kwa utayari mwaliko wa kuhudhuria. Waliihesabu kuwa pendeleo kufurahia pindi hiyo pamoja na ndugu na dada Wakristo ambao kwa miongo ya miaka walionyesha uaminifu-mshikamanifu kwa Yehova wajapokabiliwa na mnyanyaso mkali.

      Katika 1990 na 1991 pia, mikusanyiko mingine ilifanywa kotekote katika Ulaya Mashariki. Baada ya makusanyiko manne ya huko kufanywa katika Hungaria katika 1990, mipango ilifanywa kwa ajili ya mkusanyiko wa kimataifa kwenye Népstadion katika Budapest katika 1991. Waliohudhuria walikuwa 40,601 kutoka nchi 35. Kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka 40, Mashahidi wa Yehova waliweza kufanya mikusanyiko ya peupe katika Rumania katika 1990. Mfululizo wa makusanyiko kotekote nchini, na baadaye mikusanyiko miwili mikubwa, ilifanywa mwaka huo. Kulikuwa na mikusanyiko minane zaidi katika 1991, kukiwa na hudhurio la 34,808. Katika 1990, katika ile iliyokuwa Yugoslavia, mikusanyiko ilifanywa katika kila mojawapo jamhuri zilizoifanyiza nchi hiyo. Mwaka uliofuata, ingawa kulikuwa na tisho la vita ya wenyewe kwa wenyewe katika nchi hiyo, Mashahidi wa Yehova 14,684 walifurahia mkusanyiko wa kimataifa katika Zagreb, jiji kuu la Kroatia. Polisi walishangaa walipoona Wakroatia, Wamontenegro, Waserbia, Waslovenia, na wengine wakikusanyika kwa amani kusikiliza programu.

      Katika ile iliyokuwa wakati huo Chekoslovakia pia, mikusanyiko ilipangwa upesi. Mkusanyiko wa kitaifa katika Prague katika 1990 ulihudhuriwa na 23,876. Wasimamizi wa stediamu walifurahi sana kwa yale waliyoona hivi kwamba waliwapa Mashahidi mahali pakubwa zaidi nchini kwa ajili ya mkusanyiko wao ujao. Kwenye pindi hiyo ya kihistoria, katika 1991, kulikuwa na wahudhuriaji wa mkusanyiko 74,587 wenye idili waliojaa Stediamu ya Strahov katika Prague. Wajumbe Wacheki na Waslovaki walifurahi na kupiga makofi kwa idili tangazo lilipotolewa juu ya kutolewa kwa New World Translation of the Holy Scriptures iliyo kamili katika lugha zao wenyewe, ili itumiwe katika huduma ya shambani na katika funzo la kibinafsi na la kutaniko.

      Ilikuwa pia wakati wa 1991 kwamba, kwa mara ya kwanza katika historia, Mashahidi wa Yehova waliweza kufanya mikusanyiko peupe katika sehemu zilizokuwa wakati huo katika Muungano wa Sovieti. Baada ya mkusanyiko katika Tallinn, Estonia, kulikuwa na mwingine katika Siberia. Minne ilifanywa katika majiji makuu katika Ukrainia, na mmoja katika Kazakhstan. Jumla ya hudhurio ilikuwa 74,252. Na kama matokeo ya kazi ya hivi karibuni ya kufanya wanafunzi ya Mashahidi wa Yehova katika maeneo hayo, 7,820 walijitokeza kwa ajili ya uzamisho wa maji. Huo haukuwa uamuzi wa kihisiamoyo uliofanywa kwa sababu walihisi wamechochewa na mkusanyiko. Waliotaka kubatizwa walikuwa wametayarishwa kwa uangalifu kimbele kwa kipindi cha miezi mingi—au miaka katika visa vingine.

  • Sehemu ya 5—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Wengi Sasa Wanataka Kusikiliza

      Mashahidi walipofanya mikusanyiko katika ile iliyokuwa wakati huo U.S.S.R. katika 1991, umma ulikuwa na fursa ya kuwajua vema zaidi. Wao waliitikiaje? Katika Lviv, Ukrainia, ofisa mmoja wa polisi alimwambia mmoja wa wahudhuriaji wa mkusanyiko: “Mnajua sana kufundisha wengine yale yaliyo mema, mnasema juu ya Mungu, na hamjiingizi katika jeuri. Tulikuwa tukizungumza juu ya kwa nini tulikuwa tukiwanyanyasa, na tukafanya mkataa kwamba hatukuwa tumewasikiliza na hatukuwa tumejua lolote kuwahusu.” Lakini sasa wengi walikuwa wakisikiliza, na Mashahidi wa Yehova walitaka kuwasaidia.

  • Sehemu ya 5—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Kisha, katika 1992 mkusanyiko wa kimataifa wenye kutokeza ulifanywa katika St. Petersburg, jiji la pili kwa ukubwa katika Urusi. Karibu 17,000 kati ya wajumbe walitoka nchi 27 nje ya Urusi. Utangazaji mkubwa wa mkusanyiko huo ulifanywa. Kati ya wale waliokuja walikuwa watu ambao hawakuwa wamepata kusikia juu ya Mashahidi wa Yehova. Hudhurio lilifikia kilele cha 46,214. Wajumbe walikuwa wametoka sehemu zote za Urusi, wengine wao kutoka mbali sana mashariki kama Kisiwa cha Sakhalin, karibu na Japani. Vikundi vikubwa vilitoka Ukrainia, Moldova, na nchi nyinginezo ambazo hapo awali zilikuwa sehemu ya U.S.S.R. Walikuja na habari njema. Ripoti zilionyesha kwamba makutaniko mbalimbali katika majiji kama vile Kiev, Moscow, na St. Petersburg yalikuwa na wastani wa hudhurio kwenye mikutano yayo ambayo ilikuwa mara mbili au zaidi ya idadi ya Mashahidi. Watu wengi waliotaka Mashahidi wa Yehova wajifunze nao Biblia walilazimika kuwekwa kwenye orodha ya wanaongojea. Kutoka Latvia, wajumbe 600 walikuwa wamekuja na hata wengi zaidi kutoka Estonia. Kutaniko katika St. Petersburg lilikuwa na zaidi ya watu mia moja waliokuwa tayari kubatizwa kwenye mkusanyiko. Wengi wa wale wanaoonyesha kupendezwa ni vijana au watu wenye masomo ya juu. Kwelikweli, kazi kubwa ya mavuno ya kiroho inaendelea katika eneo hilo kubwa ambalo kwa muda mrefu lilionwa na ulimwengu kuwa ngome ya wasioamini kuwako kwa Mungu!

  • Sehemu ya 5—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Picha katika ukurasa wa 504]

      Baadhi ya wanaotaka kubatizwa katika Chorzów, Poland, katika 1989

  • Sehemu ya 5—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya Dunia
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Picha katika ukurasa wa 506]

      Baadhi ya Mikusanyiko ya Kihistoria Katika 1991

      Prague, Chekoslovakia

      Tallinn, Estonia (kulia)

      Zagreb, Kroatia (kulia)

      Budapest, Hungaria (juu)

      Baia-Mare, Rumania (kulia)

      Usolye-Sibirskoye, Urusi (chini)

      Alma-Ata, Kazakhstan (juu)

      Kiev, Ukrainia (kushoto)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki