-
Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni PoteMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Katika Ekuado, wakati dereva wa basi alipoanza kuendesha basi kwa ghafula, Zola Hoffman, aliyekuwa amesimama ndani ya basi, alitupwa kinyumenyume na kuanguka mapajani mwa mwanamume mmoja. Huku akiona aibu, alijaribu kuomba msamaha. Lakini lile alilosema lilikuwa, “Con su permiso” (Ukiniruhusu). Wakati mwanamume yule kwa ucheshi alipojibu, “Haya basi, endelea kuketi, Bibi,” abiria wale wengine waliangua kicheko.
-
-
Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni PoteMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Ekuado, El Salvador, Honduras, Nikaragua, Ethiopia, Gambia, Liberia, Kambodia, Hong Kong, Japani, na Vietnam. Lakini hakukuwa na Shahidi wa Yehova yeyote aliyekuwa akiripoti utendaji katika nchi hizo wakati wahitimu wamishonari wa Shule ya Gileadi walipowasili. Mahali ilipowezekana, wamishonari walianza kueneza nchi nzima kwa utaratibu, wakikaza fikira kwanza kwenye majiji makubwa zaidi. Hawakuangusha fasihi tu na kusonga mbele, kama walivyofanya makolpota zamani. Kwa saburi waliwarudia waliopendezwa, wakaongoza mafunzo ya Biblia pamoja nao, na kuwazoeza katika huduma ya shambani.
-