Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Maktaba ya Aleksandria Yajengwa Upya
    Amkeni!—2005 | Januari 8
    • Maktaba ya Aleksandria Yajengwa Upya

      ILIKUWA mojawapo ya maktaba maarufu zaidi wakati huo. Ilifanya jiji la Aleksandria huko Misri liwe kituo muhimu cha wasomi maarufu. Kutoweka kwa njia isiyojulikana kwa maktaba hiyo pamoja na maandishi yake muhimu kuliathiri sana elimu na maendeleo. Sasa, maktaba hiyo kubwa imejengwa upya.

      Jengo jipya la maktaba maarufu ya Aleksandria halina kifani. Jumba kuu la Bibliotheca Alexandrina, kama vile maktaba hiyo mpya inavyoitwa, linafanana na ngoma kubwa iliyoegemea upande. Paa yake iliyotengenezwa kwa glasi na alumini (1)—ambayo ina ukubwa unaokaribia kulingana na ule wa viwanja viwili vya mpira—ina madirisha yaliyoelekea kaskazini ambayo hupenyeza nuru kwenye jumba kuu la kusomea (2). Jengo hilo lina sehemu kuu zilizotengwa kwa ajili ya umma na sehemu fulani yake iko chini ya usawa wa bahari. Paa yake inayometameta yenye umbo la duara, imeegemea upande na inatoka ardhini hadi kwenye orofa ya saba. Kutoka mbali, paa hiyo inapopigwa na mwangaza wa jua hufanana na jua linalochomoza.

      Ukuta wa nje wa jengo hilo umejengwa kwa mawe ya matale na una michongo ya herufi za lugha za kale na za kisasa (3). Herufi hizo zilizopangwa kama ngazi huwakilisha mambo muhimu yaliyochangia ukuzi wa ujuzi.

      Jumba la kusomea lenye sehemu kadhaa zilizojengwa kama ngazi linafanyiza sehemu kubwa ya jengo hilo (4). Chini ya jengo hilo kuna sehemu inayoweza kutoshea vitabu 8,000,000. Pia jengo hilo lina sehemu za maonyesho, majumba ya hadhara, vifaa maalumu kwa ajili ya wale wasioweza kuona (5), na kitufe kinachofanana na setilaiti iliyo angani (6). Vilevile kuna mifumo tata ya kompyuta na mifumo ya kuzima moto katika jengo hilo la kisasa la hali ya juu.

  • Maktaba ya Aleksandria Yajengwa Upya
    Amkeni!—2005 | Januari 8
    • Kurudisha Fahari ya Maktaba Hiyo ya Kale

      Maktaba iliyojengwa upya ilifunguliwa mnamo Oktoba 2002, nayo ina vitabu 400,000. Mifumo tata ya kompyuta huwawezesha watu kuchunguza maktaba nyinginezo. Vitabu vingi ni vya utamaduni wa watu wanaoishi mashariki ya Mediterania. Maktaba ya Aleksandria, inayoweza kutoshea vitabu 8,000,000, itaongeza fahari ya jiji la Aleksandria.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki