-
Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya KweliMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Katika 1876, Russell alipokuwa amesoma kwa mara ya kwanza nakala ya Herald of the Morning, alikuwa amejifunza kwamba kulikuwa kikundi kingine ambacho wakati huo kiliamini kwamba kurudi kwa Kristo kungekuwa kusikoonekana na ambacho kilishirikisha kurudi huko na baraka kwa ajili ya familia zote za dunia. Kutokana na Bw. Barbour, mhariri wa kichapo hicho, Russell akaja pia kushawishwa kwamba kuwapo kusikoonekana kwa Kristo kulikuwa kumeanza katika 1874.i
-
-
Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya KweliMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
i Hilo liliongozwa na imani ya kwamba mileani ya saba ya historia ya kibinadamu ilikuwa imeanza katika 1873 na kwamba kipindi cha kutokuwa na upendeleo wa kimungu (cha urefu sawa na kipindi kilichotangulia kilichofikiriwa kuwa cha upendeleo) juu ya Israeli wa asili kingekoma katika 1878. Kronolojia hiyo ilikuwa na kosa kwa sababu ya kutegemea tafsiri isiyo sahihi ya Matendo 13:20 katika King James Version, imani ya kwamba kulikuwa kosa la kunakili kwenye 1 Wafalme 6:1, na kushindwa kufikiria kronolojia ya Kibiblia katika kuweka tarehe za milki za wafalme wa Yuda na wa Israeli. Uelewevu ulio wazi zaidi wa kronolojia ya Biblia ulitangazwa katika 1943, katika kitabu “The Truth Shall Make You Free,” halafu ukafanywa kuwa bora mwaka uliofuata katika kitabu “The Kingdom Is at Hand,” na pia katika vichapo vya baadaye.
-