Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kielelezo cha Kujidhabihu na cha Uaminifu-Mshikamanifu
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Novemba 1
    • Miaka sita baadaye, wakati wa Eliya kuondoka ukafika. Simulizi la kuondoka kwake limeitwa “mojawapo ya masimulizi yenye kuvutia zaidi” katika Maandiko ya Kiebrania.

      Eliya Ajitayarisha Kuondoka

      Eliya alitamani kuzuru Betheli, Yeriko, na Yordani kwa mara ya mwisho. Ziara hiyo ingehusisha kutembea kilometa nyingi, wakitembea baadhi ya hizo kupitia maeneo ya mlima yenye mashimo-mashimo. Kwenye kila kituo cha hiyo safari, Eliya alimtia moyo Elisha abaki hapo. Lakini Elisha alisisitiza kuendelea kuwa na bwana-mkubwa wake hadi mwisho.—2 Wafalme 2:1, 2, 4, 6.

      Walipokuwa Betheli na Yeriko, “wana wa manabii” walimkaribia Elisha.a “Je! unajua ya kuwa BWANA atamwondoa bwana wako leo, asiwe mkubwa wako?” wakamwuliza. “Naam najua,” akajibu. “Nyamazeni.”—2 Wafalme 2:3, 5.

      Kisha Eliya na Elisha wakaondoka kwenda Mto Yordani. Walipofika Yordani, Eliya alifanya muujiza huku wana wa manabii wapatao 50 wakitazama kwa mbali. “Eliya akalitwaa vazi lake la juu, akalikunja, akayapiga maji, yakagawanyika huku na huku, na hao wawili wakavuka pakavu.”—2 Wafalme 2:8.

      Mara walipokuwa wamevuka, Eliya akamwambia Elisha hivi: “Omba kwangu lo lote utakalo nikutendee, kabla sijaondolewa kwako.” Elisha akaomba “sehemu maradufu” ya roho ya Eliya—yaani, fungu maradufu ambalo kwa kawaida lingestahili mwana mzaliwa wa kwanza. Kwa kweli, Elisha alikuwa amemheshimu Eliya kama ambavyo mwana mzaliwa wa kwanza angemheshimu baba yake. Zaidi ya hayo, alitiwa-mafuta kuwa mwandamizi wa Eliya akiwa nabii wa Yehova katika Israeli. Kwa hiyo ombi lake halikuwa la ubinafsi wala lisilofaa. Hata hivyo, akijua kwamba Yehova pekee ndiye angeweza kuidhinisha ombi hilo, Eliya alijibu kwa kiasi hivi: “Umeomba neno gumu.” Kisha akaongeza hivi: “Ukiniona nitakapoondolewa kwako, utalipata; la hukuniona, hulipati.”—2 Wafalme 2:9, 10; Kumbukumbu la Torati 21:17.

      Hapana shaka Elisha aliazimia zaidi kuliko wakati mwingine wowote kushikamana kwa ukaribu na bwana-mkubwa wake. Kisha, kukatokea “gari la moto, na farasi wa moto.” Mbele ya macho ya Elisha yaliyoshtushwa, Eliya alipeperushwa na upepo wa kisulisuli—akahamishwa kimuujiza hadi mahali pengine.b Elisha alichukua vazi rasmi la Eliya, akatembea kurudi kwenye ukingo wa Mto Yordani. Akayapiga maji, akisema hivi: “Yuko wapi BWANA, Mungu wa Eliya?” Maji yaligawanyika, yakitoa uthibitisho ulio wazi kwamba Elisha alikuwa na utegemezo wa kimungu akiwa mwandamizi wa Eliya.—2 Wafalme 2:11-14.

  • Kielelezo cha Kujidhabihu na cha Uaminifu-Mshikamanifu
    Mnara wa Mlinzi—1997 | Novemba 1
    • Elisha alishikamana na Eliya hadi mwisho. Alikataa kumwacha huyo nabii mzee zaidi hata alipotolewa fursa ya kufanya hivyo. Hapana shaka, ule uhusiano wa karibu aliokuwa amekuza pamoja na Eliya ulifanya upendo huo wenye uaminifu-mshikamanifu uwe raha. Leo, watumishi wa Mungu hujitahidi kuimarisha uhusiano wao na Mungu na kuwa na ukaribu zaidi na waamini wenzao. Kifungo chenye ukaribu cha muungano kitabarikiwa, kwa maana Biblia yasema hivi juu ya Yehova: “Kwa mtu mwenye uaminifu-mshikamanifu utatenda kwa uaminifu-mshikamanifu.”—2 Samweli 22:26, NW.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki