Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Unaweza Kutumika Mahali Penye Uhitaji Mkubwa Zaidi wa Wahubiri?
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 15
    • Je, Unaweza Kutumika Mahali Penye Uhitaji Mkubwa Zaidi wa Wahubiri?

      “Tuliishi raha mustarehe nchini Marekani lakini tulikuwa na wasiwasi kwamba hali ya kutafuta sana mali katika eneo hilo ingekuwa na uvutano mbaya kwetu na kwa wana wetu wawili. Zamani mimi na mke wangu tulikuwa wamishonari, na tulitaka kufurahia tena maisha hayo rahisi lakini yenye furaha.”

      MWAKA wa 1991, tamaa hiyo iliwachochea Ralph na Pam kuandikia ofisi kadhaa za tawi na kueleza kwamba walitamani kutumika mahali penye uhitaji mkubwa zaidi wa wahubiri wa Ufalme. Ofisi ya tawi ya Mexico iliwajibu kwamba kulikuwa na uhitaji mkubwa sana wa wahubiri wa Ufalme wanaoweza kuwahubiria watu wanaozungumza Kiingereza nchini humo. Ofisi hiyo ya tawi ilisema kwamba kwa kweli eneo hilo ni ‘jeupe kwa ajili ya kuvunwa.’ (Yoh. 4:35) Muda si muda, Ralph na Pam, pamoja na wana wao wawili wenye umri wa miaka 8 na 12, walikubali mwaliko huo wakaanza kujitayarisha kuhamia Mexico.

      Eneo Kubwa Sana

      Ralph anasema hivi: “Kabla ya kuhama Marekani, ndugu na dada fulani wenye nia nzuri walituambia hivi: ‘Ni hatari sana kuhamia nchi nyingine!’ ‘Mtafanya nini mkipatwa na ugonjwa?’ ‘Kwa nini mnahamia eneo la watu wanaozungumza Kiingereza? Watu hao wanaozungumza Kiingereza hawatapendezwa na kweli!’ Hata hivyo, tuliazimia kwenda. Bila shaka, uamuzi wetu wa kuhama haukuwa wa kushtukia tu. Kwa miaka mingi tulikuwa tukipanga kuhama. Tuliepuka kuwa na madeni ya muda mrefu, tuliweka kando kiasi fulani cha pesa, na tulizungumza mara nyingi tukiwa familia kuhusu matatizo ambayo tungekabili tukihama.”

      Kwanza, Ralph na familia yake walitembelea ofisi ya tawi ya Mexico. Katika ofisi hiyo, ndugu waliwaonyesha wageni hao ramani ya nchi yote ya Mexico na kuwaambia hivi: “Hili ndilo eneo lenu!” Familia hiyo iliamua kuishi San Miguel de Allende, mji wenye wageni wengi, ulio umbali wa kilomita 240 kaskazini-magharibi ya jiji la Mexico City. Baada ya miaka mitatu kupita, kutaniko la Kiingereza lenye wahubiri 19 lilianzishwa katika mji huo. Hilo ndilo lililokuwa kutaniko la kwanza la Kiingereza katika Mexico—lakini kulikuwa na kazi nyingi zaidi iliyowangoja.

      Inakadiriwa kwamba Wamarekani milioni moja hivi wanaishi katika nchi ya Mexico. Kwa kuongezea, kuna wanafunzi na wataalamu wengi wa Mexico ambao wanazungumza lugha ya Kiingereza ikiwa lugha yao ya pili. Ralph anaeleza hivi: “Tulisali ili tupate wafanyakazi zaidi. Sikuzote tulikuwa na chumba cha ziada cha kulala katika nyumba yetu kwa ajili ya akina ndugu na dada waliokuja katika eneo letu ili ‘kuipeleleza nchi.’”—Hes. 13:2.

      Waliishi Maisha Rahisi ili Wapanue Huduma Yao

      Muda si muda, ndugu na dada zaidi waliotaka kupanua huduma yao walifika. Kati yao ni Bill na Kathy kutoka Marekani. Tayari walikuwa wametumikia kwa miaka 25 katika maeneo yenye uhitaji mkubwa wa wahubiri. Walikuwa wakifikiria kujifunza Kihispania, lakini mipango yao ilibadilika baada ya kuhamia mji wa Ajijic kwenye ufuo wa Ziwa Chapala. Watu wengi waliostaafu kutoka Marekani wanapenda kuishi katika mji huo. Bill anaeleza, “Katika mji wa Ajijic tulijitahidi sana kuwatafuta watu wanaozungumza Kiingereza ambao walitaka kujifunza kweli.” Kwa muda wa miaka miwili tangu walipofika katika mji huo, Bill na Kathy walifurahi kuona kutaniko la pili la Kiingereza likianzishwa nchini Mexico.

  • Je, Unaweza Kutumika Mahali Penye Uhitaji Mkubwa Zaidi wa Wahubiri?
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Aprili 15
    • Patrick na Roxanne kutoka katika jimbo la Texas huko Marekani walisisimuka walipopata habari kuhusu eneo la karibu la kimishonari lenye watu wanaozungumza Kiingereza. Patrick anasema hivi: “Baada ya kutembelea Monterrey, mji ulio kaskazini-mashariki mwa Mexico, tulihisi kwamba Yehova alikuwa akituelekeza huko ili tusaidie.” Baada ya siku tano, walifaulu kuuza nyumba yao huko Texas nao ‘wakavuka na kuingia Makedonia.’ (Mdo. 16:9) Kupata riziki nchini Mexico si rahisi, lakini katika miaka miwili tu, walifurahi kuona kikundi kidogo cha Mashahidi 17 kikipanuka na kuwa kutaniko lenye wahubiri 40.

      Jeff na Deb ni wenzi wa ndoa ambao pia walirahisisha maisha yao ili wapanue huduma yao. Waliuza nyumba yao kubwa huko Marekani na kuhamia nyumba ndogo huko Cancún, jiji lililo kwenye pwani ya mashariki ya Mexico. Zamani, walizoea kuhudhuria makusanyiko katika majumba ya kisasa yenye starehe karibu na nyumba yao. Sasa walilazimika kusafiri kwa muda wa saa nane ili kuhudhuria kusanyiko la karibu la Kiingereza, ambalo lilifanyiwa katika uwanja usio na paa. Lakini waliridhika sana walipoona kutaniko lenye wahubiri 50 likianzishwa huko Cancún.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki