-
Yajapokuwa Majaribu, Shikeni Imani Yenu!Mnara wa Mlinzi—1997 | Novemba 15
-
-
Tukiwa Wakristo, sisi pia tunanyanyaswa, nasi ‘hukutana na majaribu ya namna mbalimbali.’ Lakini tukikumbuka kwamba majaribu yavumiliwayo huitia nguvu imani yetu, ‘tutafikiria yote kuwa shangwe’ yatupatapo. Tukidumisha uaminifu-maadili wetu kwa Mungu wakati wa majaribu, kufanya hivyo kutatuletea furaha inayodumu.
5. Huenda majaribu yetu yakatia ndani nini, na ni nini hutukia tuyavumiliapo kwa mafanikio?
5 Majaribu yetu yatia ndani majanga yawapatayo wanadamu kwa ukawaida. Kwa kielelezo, huenda afya mbaya ikatusumbua. Mungu hafanyi maponyo ya kimuujiza sasa, lakini yeye hujibu sala zetu ili kupata hekima na nguvu zihitajiwazo ili kushughulika na ugonjwa. (Zaburi 41:1-3) Pia twateseka kwa sababu ya uadilifu tukiwa Mashahidi wa Yehova wanyanyaswao. (2 Timotheo 3:12; 1 Petro 3:14) Tuvumiliapo majaribu hayo kwa mafanikio, imani yetu yathibitishwa, ikipata kuwa yenye ‘ubora uliojaribiwa.’ Na imani yetu ishindapo, hilo “hutokeza uvumilivu.” Imani iliyofanywa kuwa yenye nguvu zaidi kupitia majaribu itatusaidia kuvumilia mitihani ya wakati ujao.
6. “Uvumilivu [huwaje] na kazi yao ikiwa kamili,” na ni hatua gani zenye kutumika ziwezazo kuchukuliwa tukiwa chini ya jaribu?
6 “Lakini,” asema Yakobo, “acheni uvumilivu uwe na kazi yao ikiwa kamili.” Tukiruhusu jaribu liendelee bila kujaribu kulikomesha upesi kwa njia isiyo ya Kimaandiko, uvumilivu utafanya “kazi” ya kutufanya tuwe Wakristo kamili, tusiokosa imani. Bila shaka, jaribu likifunua udhaifu fulani, twapaswa kutafuta msaada wa Yehova ili kuushinda. Vipi ikiwa jaribu ni kishawishi cha kushiriki katika ukosefu wa adili katika ngono? Acheni tusali juu ya tatizo hilo kisha tutende kupatana na sala zetu. Huenda tukahitaji kubadili mahali pa kazi yetu ya kuajiriwa au kuchukua hatua nyingine ili kudumisha uaminifu-maadili kwa Mungu.—Mwanzo 39:7-9; 1 Wakorintho 10:13.
-
-
Yajapokuwa Majaribu, Shikeni Imani Yenu!Mnara wa Mlinzi—1997 | Novemba 15
-
-
Wenye Furaha Ni Wale Wanaovumilia Jaribu
11. Washikao imani wakabilipo majaribu wana matazamio gani?
11 Tuwe matajiri au maskini, twaweza kuwa wenye furaha ikiwa tu twavumilia majaribu yetu. (Yakobo 1:12-15) Tukivumilia majaribu tukidumisha imani yetu, twaweza kutamkwa kuwa wenye furaha, kwa kuwa kuna shangwe katika kufanya lililo sawa machoni pa Mungu. Kwa kushika imani yao hadi kifo, Wakristo wa kuzaliwa kwa roho hupokea “taji la uhai,” hali ya kutokufa mbinguni. (Ufunuo 2:10; 1 Wakorintho 15:50) Ikiwa tuna matumaini ya kidunia na twadumisha imani yetu katika Mungu, twaweza kutazamia uhai udumuo milele kwenye dunia iliyo paradiso. (Luka 23:43; Waroma 6:23) Jinsi Yehova alivyo mwema kwa wote ambao hudhihirisha imani kwake!
-