-
Enoki—Asiye na Hofu Kujapokuwa MagumuMnara wa Mlinzi—1997 | Januari 15
-
-
Je, Enoki Alienda Mbinguni?
“Kwa imani Enoki alihamishwa ili asione kifo.” Katika kutafsiri kwazo sehemu hiyo ya Waebrania 11:5, tafsiri fulani za Biblia huonyesha kwamba Enoki hakufa kihalisi. Kwa kielelezo, A New Translation of the Bible, ya James Moffatt, hutaarifu hivi: “Ni kwa imani kwamba Enoki alichukuliwa kwenda mbinguni hivi kwamba hakufa kamwe.”
Hata hivyo, miaka ipatayo 3,000 baada ya siku ya Enoki, Yesu Kristo alitaarifu hivi: “Hakuna mtu ambaye amepaa kuingia mbinguni ila yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, Mwana wa binadamu.” (Yohana 3:13) The New English Bible husomeka hivi: “Hakuna yeyote aliyekwenda mbinguni wakati wowote isipokuwa yule aliyeshuka kutoka mbinguni, Mwana wa Binadamu.” Wakati Yesu alipotoa taarifa hiyo, hata hakuwa amepaa mbinguni.—Linganisha Luka 7:28.
Mtume Paulo hutaarifu kwamba Enoki na wengine wafanyizao wingu kubwa ya mashahidi wa kabla ya Ukristo ‘wote walikufa’ na “hawakupata utimizo wa ahadi.” (Waebrania 11:13, 39) Kwa sababu gani? Kwa sababu wanadamu wote, kutia ndani Enoki, wamerithi dhambi kutoka kwa Adamu. (Zaburi 51:5; Waroma 5:12) Njia pekee ya wokovu ni kupitia dhabihu ya fidia ya Kristo Yesu. (Matendo 4:12; 1 Yohana 2:1, 2) Katika siku ya Enoki fidia hiyo haikuwa imelipwa bado. Kwa hiyo, Enoki hakuenda mbinguni, lakini amelala katika kifo akingojea ufufuo duniani.—Yohana 5:28, 29.
-
-
Enoki—Asiye na Hofu Kujapokuwa MagumuMnara wa Mlinzi—1997 | Januari 15
-
-
Mungu Alimtwaa Enoki —Jinsi Gani?
Yehova hakumruhusu Shetani au watumishi wake wa kidunia wamwue Enoki. Badala ya hivyo, rekodi yenye kupuliziwa husema hivi: “Mungu alimtwaa.” (Mwanzo 5:24) Mtume Paulo hufafanua mambo hivi: “Kwa imani Enoki alihamishwa ili asione kifo, naye hakupatikana mahali popote kwa sababu Mungu alikuwa amemhamisha; kwa maana kabla ya uhamisho wake alikuwa na ushahidi kwamba alikuwa amempendeza Mungu vema.”—Waebrania 11:5.
Enoki ‘alihamishwaje ili asione kifo?’ Au kama ambavyo imetafsiriwa katika tafsiri ya Habari Njema kwa Watu Wote, Enoki ‘alichukuliwaje na Mungu asipate kufa’? Mungu alikatiza kwa amani uhai wa Enoki, akimwepusha asipatwe na maumivu makali ya ghafula ya kifo kutokana na ama ugonjwa ama jeuri mikononi mwa maadui wake. Ndiyo, Yehova alifupiza uhai wa Enoki alipokuwa na umri wa miaka 365—alikuwa kijana akilinganishwa na watu walioishi wakati wake.
Enoki alitolewaje “ushahidi kwamba alikuwa amempendeza Mungu vema”? Alikuwa na uthibitisho gani? Yamkini, Mungu alimtia Enoki katika njozi, kama vile mtume Paulo ‘alivyonyakuliwa’ au kuhamishwa, yaonekana akipokea ono juu ya paradiso ya kiroho ya wakati ujao ya kutaniko la Kikristo. (2 Wakorintho 12:3, 4) Ushahidi, au uthibitisho, kwamba Enoki alikuwa amekuwa mwenye kumpendeza Mungu ungaliweza kuhusisha ono juu ya Paradiso ya kidunia ijayo ambamo wale wote wenye kuishi wataunga mkono enzi kuu ya Mungu. Huenda ikawa ni wakati Enoki alipokuwa akipatwa na ono lenye furaha nyingi kwamba Mungu alimtwaa katika kifo kisicho na maumivu kulala hadi siku ya ufufuo. Yaonekana kwamba, kama vile katika kisa cha Musa, Yehova aliondolea mbali mwili wa Enoki, kwa kuwa ‘haukupatikana mahali popote.’—Waebrania 11:5; Kumbukumbu la Torati 34:5, 6; Yuda 9.
-