-
Aliwatetea Watu wa MunguMnara wa Mlinzi—2011 | Oktoba 1
-
-
Mwanamume aliyeitwa Hamani alipewa cheo cha juu katika utawala wa Ahasuero. Mfalme alimchagua Hamani kuwa waziri mkuu, hivyo akawa mshauri wake mkuu na mtu wa pili kwa cheo katika milki yake. Hata mfalme aliagiza kwamba kila mtu amwinamie anapomwona. (Esta 3:1-4) Sheria hiyo ilitokeza tatizo kubwa kwa Mordekai. Alijua kwamba alipaswa kumtii mfalme, lakini hangefanya hivyo ikiwa jambo hilo lingemvunjia Mungu heshima. Ona kwamba Hamani alikuwa “Mwagagi.” Hilo linamaanisha kwamba alikuwa mzao wa Agagi, mfalme wa Waamaleki ambaye aliuawa na Samweli, nabii wa Mungu. (1 Samweli 15:33) Waamaleki walikuwa waovu sana na hivyo wakawa maadui wa Yehova na Waisraeli. Taifa la Waamaleki lilihukumiwa na Mungu.b (Kumbukumbu la Torati 25:19) Myahudi mwaminifu angewezaje kumwinamia Mwamaleki mwenye mamlaka? Mordekai hangefanya hivyo. Alisimama imara. Leo pia, wanaume na wanawake wenye imani wamehatarisha maisha yao kwa kutii kanuni hii: “Lazima tumtii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.”—Matendo 5:29.
Jambo hilo lilimkasirisha sana Hamani. Lakini hangetosheka kwa kumwangamiza Mordekai peke yake. Alitaka kuwaangamiza watu wote wa Mordekai! Hamani alizungumza na mfalme na kufanya Wayahudi waonekane kuwa watu wabaya. Bila kuwataja Wayahudi moja kwa moja, alisema wao si watu wa maana na kwamba “wa[me]tawanyika na kujitenga kati ya vikundi vya watu.” Hata alisema kwamba hawakuheshimu sheria za mfalme; hivyo, walikuwa waasi hatari. Kisha, akajitolea kuchanga kiasi kikubwa cha pesa kwa hazina ya mfalme ili kulipia kazi ya kuwaua Wayahudi wote katika milki hiyo.c Basi Ahasuero akampa Hamani pete yake ya kifalme ya mhuri ili atie mhuri amri yoyote aliyotaka itekelezwe.—Esta 3:5-10.
-
-
Aliwatetea Watu wa MunguMnara wa Mlinzi—2011 | Oktoba 1
-
-
b Yaelekea Hamani alikuwa mmoja wa wazao wa mwisho-mwisho wa Waamaleki, kwa sababu wale ‘waliobaki’ waliangamizwa katika siku za Mfalme Hezekia.—1 Mambo ya Nyakati 4:43.
c Hamani alitoa mchango wa talanta 10,000 za fedha, kiasi ambacho leo ni sawa na mamilioni ya dola. Ikiwa Ahasuero alikuwa Shasta wa Kwanza, basi huenda pesa hizo zilimchochea akubali pendekezo la Hamani. Shasta alikuwa ametumia pesa nyingi sana alipopigana na Wagiriki katika vita vilivyosababisha uharibifu mkubwa. Labda alipigana vita hivyo kabla ya kumwoa Esta.
-