-
Filipo Ambatiza Ofisa MwethiopiaMnara wa Mlinzi—1996 | Julai 15
-
-
“Ni Nini Kinachonizuia Nisibatizwe?”
“Nakuomba,” yule Mwethiopia akamwambia Filipo, “nabii huyu; asema maneno haya kwa habari ya nani; ni habari zake mwenyewe au za mtu mwingine?” (Matendo 8:34) Kutatanika kwa Mwethiopia hakukuwa kwenye kushangaza, kwa kuwa utambulishi wa “kondoo,” au “mtumishi,” wa unabii wa Isaya ulikuwa umekuwa fumbo kwa muda mrefu. (Isaya 53:11) Lazima iwe ilikuwa wazi kama nini Filipo alipomtangazia huyo Mwethiopia “habari njema za Yesu”! Baada ya muda huyo Mwethiopia akasema: “Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?” Kwa hiyo Filipo akambatiza papo hapo.—Matendo 8:35-38.
Je, hilo lilikuwa tendo la haraka-haraka? Sivyo hata kidogo! Huyo Mwethiopia alikuwa mgeuzwa-imani Myahudi.b Kwa hiyo tayari alikuwa mwabudu wa Yehova mwenye ujuzi wa Maandiko, kutia ndani na unabii mbalimbali wa Kimesiya. Hata hivyo, ujuzi wake haukuwa kamili. Sasa kwa kuwa alikuwa amepata habari hiyo muhimu juu ya fungu la Yesu Kristo, huyo Mwethiopia alifahamu yale ambayo Mungu alitaka afanye naye alikuwa tayari kutii. Ubatizo ulifaa.—Mathayo 28:18-20; 1 Petro 3:21.
-
-
Filipo Ambatiza Ofisa MwethiopiaMnara wa Mlinzi—1996 | Julai 15
-
-
Bila shaka, wale walio wapya hawapasi kuharakishwa kwenye ubatizo. Kwanza ni lazima wapate ujuzi sahihi juu ya Yehova Mungu na juu ya Mwanae, Yesu Kristo. (Yohana 17:3) Kisha lazima watubu, waache mwenendo mbaya na kugeuka ili kujipatanisha na viwango vya Mungu. (Matendo 3:19) Hilo huchukua muda, hasa ikiwa fikira na mwenendo mbaya zimekwisha thibitika. Ingawa wapya wapaswa kuhesabu gharama ya uanafunzi wa Kikristo, baraka kubwa hutokana na kuingia katika uhusiano wa kujiweka wakfu kwa Yehova Mungu. (Linganisha Luka 9:23; 14:25-33.) Wale ambao ni Mashahidi wa Yehova huwaongoza hao wapya kwa idili kwenye tengenezo analotumia Mungu ili kutimiza mapenzi yake. (Mathayo 24:45-47) Sawa na huyo Mwethiopia, wapya hao watafurahia kujifunza na kutii yale ambayo Mungu ataka wafanye.
-