-
Ushindi wa Kisheria Baada ya Kupambana kwa Muda Mrefu!Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
-
-
“ILI KUWA USHAHIDI”
Ili kuthibitisha kwamba marufuku ya Moscow yalivunja sheria, katika Desemba (Mwezi wa 12) 2004 wanasheria wetu walitafuta msaada katika Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu. (Ona sanduku “Kwa Nini Uamuzi wa Urusi Ulichunguzwa Tena Huko Ufaransa?” kwenye ukurasa wa 6.) Miaka sita baadaye, katika Juni 10, 2010, Mahakama ilifanya uamuzi wa pamoja ambao ulionyesha kwamba Mashahidi wa Yehova hawana hatia hata kidogo!e Mahakama hiyo ilichunguza mashtaka yote ambayo yalitolewa juu yetu na ikapata kwamba hayakuwa na msingi wowote. Ilisema pia kwamba Urusi ilikuwa na daraka la kisheria la “kuzuia uvunjaji wa sheria ambao Mahakama hiyo ilipata na kurekebisha mambo kadiri iwezekanavyo.”—Ona sanduku “Uamuzi wa Mahakama,” kwenye ukurasa wa 8.
Maamuzi ya Mahakama hiyo ambayo yanaeleza waziwazi jinsi Makubaliano au Mkataba wa Ulaya unavyolinda kazi ya Mashahidi wa Yehova hayahusu tu Urusi bali pia mataifa mengine 46 ambayo ni sehemu ya Baraza la Ulaya. Zaidi ya hayo, kwa sababu ya maelezo yake ya ndani sana kuhusu uchunguzi wa kisheria na mambo ya hakika, mambo hayo yatasomwa kwa makini na wasomi wa mambo ya sheria, mahakimu, wale wanaotunga sheria, na wataalamu wa haki za kibinadamu ulimwenguni pote. Kwa nini? Ili kufikia uamuzi wake, Mahakama hiyo haikutaja tu maamuzi manane ambayo ilifanya zamani ambayo yanawaunga mkono Mashahidi wa Yehova bali pia ilitaja kesi tisa ambazo Mashahidi wa Yehova walishinda kabla ya hapo katika mahakama kuu zaidi huko Afrika Kusini, Argentina, Hispania, Japani, Kanada, Marekani, Uingereza, na Urusi. Maamuzi hayo pamoja na hatua ya Mahakama hiyo ya kupinga vikali sana mashtaka yaliyotolewa na kiongozi wa mashtaka wa Moscow yanawapa Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote kifaa chenye nguvu sana cha kutumia ili kutetea imani na kazi yao.
-
-
Ushindi wa Kisheria Baada ya Kupambana kwa Muda Mrefu!Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
-
-
e Mnamo Novemba 22, 2010 (22/11/2010), kikundi cha mahakimu watano wa Baraza Kuu la Mahakama ya Ulaya ya Haki za Kibinadamu kilikataa ombi la Urusi la kutaka kesi hiyo ipelekwe katika Baraza Kuu la Mahakama hiyo. Walipokataa ombi hilo, walionyesha kwamba uamuzi wa Juni 10, 2010, ulikuwa wa mwisho na hivyo unapaswa kutekelezwa.
-
-
Ushindi wa Kisheria Baada ya Kupambana kwa Muda Mrefu!Mnara wa Mlinzi—2011 | Julai 15
-
-
[Sanduku katika ukurasa wa 8]
Uamuzi wa Mahakama
Hapa chini pana mafungu matatu mafupi yanayoonyesha uamuzi uliofanywa na Mahakama.
Shtaka moja lilisema kwamba Mashahidi wa Yehova wanavunja familia. Mahakama ilifanya uamuzi uliopinga shtaka hilo. Ilisema hivi:
“Matatizo yanasababishwa na washiriki wa familia ambao si wanadini ambao wanapinga na hawako tayari kukubali na kuheshimu uhuru wa kidini wa watu wao wa ukoo na haki yao ya kufuata dini yao.”—Fungu la 111.
Mahakama hiyo pia haikupata ushahidi wa kuunga mkono shtaka la kwamba Mashahidi “wanawapofusha watu akili.” Ilisema hivi:
“Mahakama hii inashangaa kwamba mahakama za [Urusi] hazikutaja jina la mtu hata mmoja ambaye inasemekana kwamba haki yake ya kuwa na uhuru wa dhamiri ilipuuzwa kupitia mbinu hizo.”—Fungu la 129.
Shtaka lingine lilisema kwamba Mashahidi wa Yehova wanaharibu afya ya waamini kwa kutokubali kutiwa damu mishipani. Mahakama hiyo ilitoa uamuzi ambao ni kinyume. Ilisema hivi:
“Uhuru wa kukubali au kukataa matibabu fulani, au kuchagua aina nyingine ya matibabu, ni wa maana katika kanuni za uhuru wa kibinafsi na wa mtu kujiamulia mambo yake mwenyewe. Kwa mfano, mtu mzima ambaye ni mgonjwa ana uhuru wa kuamua ikiwa atakubali au hatakubali matibabu au kufanyiwa upasuaji au, kwa msingi huohuo, ana uhuru wa kuamua kama atatiwa damu mishipani.”—Fungu la 136.
-