Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezra
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Januari 15
    • Mambo Tunayojifunza:

      1:2. Mambo ambayo Isaya alitabiri miaka 200 hivi mapema yalitimia. (Isaya 44:28) Unabii unaopatikana katika Neno la Yehova hauwezi kukosa kutimia.

      1:3-6. Sawa na Waisraeli waliobaki Babiloni, Mashahidi wengi wa Yehova hawawezi kuwa wahudumu wa wakati wote au kutumikia mahali penye uhitaji mkubwa. Lakini wao huwaunga mkono na kuwatia moyo wale wanaoweza kufanya hivyo, nao hutoa michango ya hiari kuendeleza kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme na kufanya wanafunzi.

      3:1-6. Katika mwezi wa saba wa mwaka wa 537 K.W.K. (Tishri, unaolingana na Septemba/Oktoba), watu waaminifu waliorudi katika nchi yao walitoa dhabihu yao ya kwanza. Wababiloni walikuwa wameingia Yerusalemu katika mwezi wa tano (Abi, unaolingana na Julai/Agosti) wa mwaka wa 607 K.W.K., na miezi miwili baadaye jiji hilo lilikuwa ukiwa kabisa. (2 Wafalme 25:8-17) Kama ilivyokuwa imetabiriwa, ukiwa wa miaka 70 wa Yerusalemu ulimalizika kwa wakati. (Yeremia 25:11; 29:10) Jambo lolote ambalo Neno la Yehova hutabiri hutimia.

      4:1-3. Mabaki waaminifu walikataa ombi ambalo lingewafanya waanzishe mapatano ya kidini pamoja na waabudu wa uwongo. (Kutoka 20:5; 34:12) Vivyo hivyo, waabudu wa Yehova leo hawashiriki mambo yoyote ya kuchanganya ibada.

      5:1-7; 6:1-12. Yehova anaweza kuongoza mambo ili watu wake wafanikiwe.

      6:14, 22. Kufanya kazi ya Yehova kwa bidii huleta kibali na baraka zake.

      6:21. Wasamaria walioishi katika nchi ya Wayahudi na watu waliorudi ambao waliathiriwa na uvutano wa kipagani walichochewa kufanya mabadiliko maishani mwao baada ya kushuhudia maendeleo ya kazi ya Yehova. Je, hatupaswi kufanya kazi yetu tuliyogawiwa na Mungu kwa uchangamfu, kutia ndani kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme?

  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ezra
    Mnara wa Mlinzi—2006 | Januari 15
    • Mambo Tunayojifunza:

      7:10. Ezra alituwekea mfano akiwa mwanafunzi mwenye bidii na mwalimu mwenye matokeo wa Neno la Mungu. Kupitia sala, alitayarisha moyo wake kutafuta shauri katika Sheria ya Yehova. Alipofanya hivyo, Ezra alikazia uangalifu kabisa mambo ambayo Yehova alisema. Ezra alitumia mambo aliyojifunza na kuwafundisha wengine kwa bidii.

      7:13. Yehova anataka watumishi wanaojitoa kwa hiari.

      7:27, 28; 8:21-23. Ezra alimsifu Yehova, akamsihi kwa unyoofu kabla ya kufunga safari hatari ya kwenda Yerusalemu, naye alikuwa tayari kujihatarisha kwa ajili ya utukufu wa Mungu. Hivyo, alituwekea mfano bora.

      9:2. Tunapaswa kuchukua kwa uzito shauri la kuoa “katika Bwana tu.”—1 Wakorintho 7:39.

      9:14, 15. Mashirika mabaya yanaweza kutufanya tupoteze kibali cha Yehova.

      10:2-12, 44. Watu waliokuwa wamechukua wake wa kigeni walitubu kwa unyenyekevu na kurekebisha njia zao. Mtazamo wao na hatua walizochukua ni mfano bora kwetu.

      Yehova Hutimiza Ahadi Zake

      Kitabu cha Ezra ni muhimu sana kwetu! Kwa wakati unaofaa kabisa, Yehova alitimiza ahadi yake ya kuwaweka huru watu wake kutoka uhamishoni huko Babiloni na kurudisha ibada ya kweli huko Yerusalemu. Je, hilo haliimarishi imani yetu katika Yehova na katika ahadi zake?

      Fikiria mifano iliyo katika kitabu cha Ezra. Ezra na mabaki waliorudi kushiriki katika kazi ya kurudisha ibada safi huko Yerusalemu waliweka mfano bora wa kujitoa kwa Mungu. Pia, kitabu hiki kinakazia imani ya watu wa nchi za kigeni ambao walimwogopa Mungu na mtazamo wa unyenyekevu wa wakosaji waliotubu. Naam, maneno ya Ezra yaliyoandikwa kwa uongozi wa roho yanaonyesha wazi kwamba “neno la Mungu liko hai nalo lina nguvu.”—Waebrania 4:12.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki