Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Naweza Kuishije Nikiwa na Huzuni Yangu?
    Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
    • Kuongea kwaweza kuwa njia yenye kusaidia kuondosha huzuni. Baada ya kifo cha watoto wake wote kumi, pamoja na misiba mingine ya kibinafsi, Ayubu yule mzee wa ukoo wa kale alisema hivi: “Hakika nafsi yangu yahisi kukirihi kuelekea maisha yangu. Nitatoa [Kiebrania, “nitaachilia”] hangaiko langu kuhusu mwenyewe. Nitasema katika uchungu wa nafsi yangu!” (Ayubu 1:2, 18, 19; 10:1, NW) Ayubu hakuweza tena kuzuia hangaiko lake. Alilazimika kuliachilia; alihitaji ‘kunena.’ Vivyo hivyo, mtunga-drama Mwingereza Shakespeare aliandika hivi katika drama iitwayo Macbeth: “Onyesha majonzi; huzuni isiyosema manong’ono hulemea moyo nayo huupasua.”

      Kwa hiyo kuongea juu ya hisia zako pamoja na “rafiki wa kweli” atakayesikiliza kwa saburi na kwa kusikitikia kwaweza kuleta kadiri fulani ya kitulizo. (Mithali 17:17, NW) Mara nyingi kueleza maono na hisia hufanya iwe rahisi zaidi kuzielewa na kushughulika nazo kwa kufaa. Na ikiwa msikilizaji ni mtu mwingine aliyefiwa ambaye ameshughulika vya kufaa na hasara yake mwenyewe kwa mafanikio, huenda ukapata madokezo yenye kutumika juu ya jinsi ya kushughulika vya kufaa na hali yako. Mtoto wake alipokufa, mama mmoja alieleza kwa nini ilisaidia kuongea na mwanamke mwingine aliyekuwa amepatwa na hasara hiyohiyo: “Kujua kwamba mtu mwingine alikuwa amepatwa na jambo lilo hilo, alikuwa angali na afya nzuri ya kiakili na ya kihisiamoyo, na kwamba alikuwa angali anaendelea kuishi na kuwa na utaratibu fulani maishani mwake tena kuliniimarisha sana.”

      Namna gani ikiwa huhisi starehe kuongea juu ya hisia zako? Baada ya kifo cha Sauli na Yonathani, Daudi alitunga wimbo wa maombolezo ambao katika huo alimwaga huzuni yake yote. Hatimaye wimbo huo wa maombolezo ukawa sehemu ya maandishi ya kitabu cha Biblia cha Samweli wa Pili. (2 Samweli 1:17-27; 2 Mambo ya Nyakati 35:25) Vivyo hivyo, wengine huona ni rahisi zaidi kujieleza kwa kuandika. Mjane mmoja aliripoti kwamba yeye alikuwa akiandika hisia zake kisha siku kadhaa baadaye alikuwa akisoma yale aliyokuwa ameandika. Aliona hiyo kuwa njia yenye kusaidia kuondosha huzuni.

      Iwe ni kwa kuongea au kwa kuandika, kuwasilisha hisia zako kwaweza kukusaidia uondoshe huzuni yako. Kwaweza pia kuondolea mbali kutoelewana. Mama mmoja aliyefiwa aeleza hivi: “Mume wangu nami tulisikia juu ya waume na wake wengine waliotalikana baada ya kufiwa na mtoto, nasi hatukutaka hilo litupate. Kwa hiyo wakati wowote tulipokasirika, tukitaka kulaumiana, tulikuwa tukiongea juu yalo. Nafikiri tulikaribiana sana kwa kufanya hivyo.” Hivyo, kujulisha hisia zenu kwaweza kuwasaidia mwelewe kwamba hata ingawa huenda ikawa mnashiriki pamoja hasara ile ile, wengine waweza kuhuzunika kwa njia tofauti—kwa mwendo wao wenyewe na kwa njia yao wenyewe.

  • Naweza Kuishije Nikiwa na Huzuni Yangu?
    Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa
    • Kama ilivyoonyeshwa kimbele, wengine wana hisia za kuwa na hatia baada ya kufiwa na mpendwa. Hilo huenda likasaidia kueleza sababu ya ile huzuni nyingi ya yule mwanamume mwaminifu Yakobo alipofanywa aamini kwamba mwana wake Yusufu alikuwa ameuawa na “hayawani-mwitu mkali.” Yakobo mwenyewe alikuwa amemtuma Yusufu aende akachunguze hali njema ya ndugu zake. Kwa hiyo yaelekea Yakobo alisumbuliwa na hisia za kuwa na hatia, kama vile ‘Kwa nini nilimtuma Yusufu akiwa peke yake? Kwa nini nilimtuma kwenye eneo ambalo limejaa mahayawani-mwitu?’—Mwanzo 37:33-35, NW.

      Labda wewe wahisi kwamba uzembe fulani upande wako ulichangia kifo cha mpendwa wako. Kung’amua kwamba kuhisi una hatia—iliyo halisi au ya kuwaziwa tu—ni itikio la kawaida la huzuni kwenyewe kwaweza kusaidia. Hapa tena, usihisi kwamba hupaswi kuonyesha hisia hizo. Kuongea juu ya jinsi uhisivyo kwamba una hatia kwaweza kuandaa ondoleo kubwa linalohitajiwa la huzuni.

      Ingawa hivyo, ng’amua kwamba haidhuru ni kadiri gani tumpendavyo mtu mwingine, sisi hatuwezi kudhibiti maisha yake, wala hatuwezi kuzuia “wakati na tukio lisilotazamiwa” lisiwapate wale tuwapendao. (Mhubiri 9:11, NW) Ingawaje, bila shaka madhumuni yako hayakuwa mabaya. Kwa kielelezo, kwa kutofanya mpango wa kumwona daktari mapema zaidi, je, wewe ulikusudia mpendwa wako awe mgonjwa na kufa? Bila shaka sivyo! Basi, je, una hatia kwelikweli ya kusababisha kifo cha mtu huyo? La.

      Mama mmoja alijifunza kushughulika vya kufaa na hali ya kuhisi ana hatia baada ya binti yake kufa katika aksidenti ya gari. Yeye aeleza hivi: “Nilihisi nina hatia kwa sababu ya kumtuma. Lakini nikaja kung’amua kwamba kuhisi hivyo lilikuwa jambo la upuuzi. Kumtuma aende na baba yake afanye kazi fulani hakukuwa kosa. Hiyo ilikuwa aksidenti tu iliyo mbaya sana.”

      ‘Lakini kuna mambo mengi sana ambayo laiti ningalisema au kufanya,’ huenda ukasema. Ni kweli, lakini ni nani kati yetu awezaye kusema kwamba sisi tumekuwa baba, mama, au mtoto mkamilifu? Biblia hutukumbusha hivi: “Sisi sote hujikwaa mara nyingi. Ikiwa yeyote hajikwai katika neno, huyu ni mtu mkamilifu.” (Yakobo 3:2; Warumi 5:12, NW) Kwa hiyo kubali uhakika wa kwamba wewe si mkamilifu. Kuendelea kufikiri-fikiri ati “laiti tu ningalifanya hivi au vile” hakutabadili chochote, lakini huenda kwaweza kukawiza kupata kwako nafuu.

      Ikiwa una sababu nzuri za kuamini kwamba hatia yako ni halisi, isiyowaziwa tu, basi fikiria lile jambo la maana zaidi ya yote katika kutuliza hisia ya kuwa na hatia—msamaha wa Mungu. Biblia hututia moyo hivi: “BWANA, kama Wewe ungehesabu maovu, Ee Bwana, nani angesimama? Lakini kwako kuna msamaha.” (Zaburi 130:3, 4) Huwezi kurudia wakati uliopita na kubadili chochote. Lakini, waweza kumwomba Mungu msamaha kwa makosa ya wakati uliopita. Kisha nini? Ikiwa Mungu anaahidi kufuta kabisa makosa yako, je, wewe hupaswi pia kujisamehe?—Mithali 28:13; 1 Yohana 1:9.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki