-
Mkono wa Yehova WainuliwaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
[Picha katika ukurasa wa 275]
“Karamu ya vitu vinono”
-
-
Mkono wa Yehova WainuliwaUnabii wa Isaya I—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
‘Karamu kwa Mataifa Yote’
6, 7. (a) Yehova aandaa karamu ya aina gani, naye awaandalia nani? (b) Karamu aliyoitabiri Isaya yawakilisha nini?
6 Kama vile baba mwenye upendo, Yehova huwalinda na pia kuwalisha watoto wake, hasa kiroho. Baada ya kuwakomboa watu wake mwaka wa 1919, aliwaandalia karamu ya ushindi, yaani, chakula kingi cha kiroho: “Katika mlima huu BWANA wa majeshi atawafanyia mataifa yote karamu ya vitu vinono, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, karamu ya vinono vilivyojaa mafuta, karamu ya divai iliyokaa juu ya urojorojo wake, iliyochujwa sana.”—Isaya 25:6.
7 Karamu hiyo yafanyiwa katika “mlima” wa Yehova. Mlima huo ni nini? Huo ni “mlima wa nyumba ya BWANA [“Yehova,” NW]” ambao mataifa yote yanauendea “katika siku za mwisho.” Huo ni ‘mlima mtakatifu’ wa Yehova, ambako waabudu wake waaminifu hawadhuru wala hawaharibu. (Isaya 2:2; 11:9) Katika mahali hapo pa ibada palipoinuliwa, Yehova aandaa karamu ya vitu vitamu kwa ajili ya watu waaminifu. Na vitu vizuri vya kiroho vinavyoandaliwa kwa wingi sasa vyaonyesha kimbele vitu vitamu vya kimwili vitakavyoandaliwa Ufalme wa Mungu utakapokuwa serikali pekee ya wanadamu. Wakati huo njaa haitakuwepo tena. ‘Kutakuwepo wingi wa nafaka katika ardhi juu ya milima.’—Zaburi 72:8, 16.
8, 9. (a) Ni adui gani wawili wakuu wa wanadamu watakaoondolewa? Eleza. (b) Mungu atafanya nini ili kuiondoa aibu ya watu wake?
8 Wale wanaokula sasa karamu ya kiroho ambayo Mungu ameandaa wana matazamio matukufu.
-