-
Je, Uhai Wote Umetokana na Chanzo Kimoja?Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai
-
-
MICHORO YA VITABU NA SANAMU ZA SOKWE
◼ Ukweli wa mambo: Michoro katika vitabu na majumba ya makumbusho ya wale wanaoitwa eti wazazi wa kale wa mwanadamu mara nyingi huonyeshwa ikiwa na umbo la uso, rangi ya ngozi, na kiasi fulani cha nywele. Kwa kawaida michoro hiyo huonyesha “wazazi” wa zamani sana wakiwa na sura kama za nyani, na wanaodhaniwa kuwa wanakaribiana zaidi na wanadamu huonyeshwa wakiwa na umbo la uso, rangi ya ngozi, na nywele kama za mwanadamu.
Swali: Je, wanasayansi wanaweza kutengeneza upya maumbo hayo kwa kutegemea mabaki ya visukuku wanavyopata?
Jibu: Hapana. Mwaka 2003, mwanasayansi Carl N. Stephan, anayefanya kazi katika Idara ya Sayansi ya Anatomia ya Chuo Kikuu cha Adelaide, nchini Australia, aliandika hivi: “Nyuso za wazazi wa kale haziwezi kuundwa kwa usahihi au kufanyiwa majaribio.” Anasema kwamba majaribio ya aina hiyo yanayotegemea sokwe wa kisasa “yatakuwa yenye kupendelea upande mmoja, yasiyo sahihi hata kidogo, na ya ubatili.” Alikata maneno jinsi gani? “Yaelekea maumbo yoyote ya nyuso za hominidi wa kale ‘yaliyoundwa upya,’ yatakuwa yenye kupotosha.”47
-
-
Je, Uhai Wote Umetokana na Chanzo Kimoja?Maswali Matano Muhimu Kuhusu Chanzo cha Uhai
-
-
PICHA HII INA KASORO GANI?
◼ Picha za aina hii hutegemea makisio na maoni yenye kupendelea upande mmoja ya watafiti na wachoraji wala si ukweli wa mambo.51
◼ Mingi ya michoro hiyo hutegemea mafuvu nusu-nusu na meno ya hapa na pale. Si rahisi kupata mafuvu kamili wala viunzi kamili vya mifupa.
◼ Watafiti hawapatani kuhusu jinsi visukuku vya viumbe mbalimbali vinavyopaswa kuainishwa.
◼ Wachoraji hawawezi kuunda upya maumbo ya uso, rangi ya ngozi, na nywele za viumbe hao waliotoweka.
◼ Kila kiumbe kimewekwa mahali hususa katika mpangilio wa mageuzi mpaka kufikia kwa mwanadamu kwa kutegemea ukubwa wa fuvu la ubongo wake. Hilo linafanywa licha ya uthibitisho wa kwamba ukubwa wa ubongo si njia inayotegemeka ya kuamua uwezo wa akili.
-