Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Vijana Hupendezwa na Dini Kadiri Gani?
    Amkeni!—1998 | Agosti 8
    • Vijana Hupendezwa na Dini Kadiri Gani?

      NA MLETA-HABARI WA AMKENI! KATIKA UFARANSA

      KWA vijana 750,000 waliohudhuria, hii ingekuwa jioni ya kufurahisha sana. Walipunga bendera, wakaimba na kushangilia. Miale na fataki zilirushwa hewani na wanamuziki wakachangamsha umati. Hali ilifanana na “disko kubwa sana iliyopangwa kwa haraka.” Hatimaye, kukiwa na vigelegele vya usifaji, mtu waliyekuwa wamemngoja akatokea jukwaani.

      Je, huu ulikuwa mwanzo wa safari ya kuzuru ulimwengu wote ya bendi ya roki? La. Ulikuwa mkutano wa kidini uliohudhuriwa na umati mkubwa katika Paris wakati wa Siku za Vijana Wakatoliki Ulimwenguni, na mtu mwenyewe alikuwa Papa John Paul wa Pili!

      Kwa watu wengine, kupendezwa kwa vijana na misherehekeo ya kidini kama hii laonekana kuwa jambo la kustaajabisha. Lakini sasa vyombo vya habari vinazungumzia hali ya vijana kupenda dini tena.

  • Vijana Hupendezwa na Dini Kadiri Gani?
    Amkeni!—1998 | Agosti 8
    • Jitihada ya Vijana ya Kuchunguza Dini

      Dini zinapata ugumu wa kuvutia vijana. Kasisi Mfaransa aliuliza umati uliokuwa ukihudhuria Siku za Vijana Wakatoliki Ulimwenguni katika Paris hivi: “Vijana hawa wametoka wapi? Hakuna vijana katika makanisa yangu. Siwaoni kamwe.” Ili kuvutia na kudumisha uangalifu wa vijana, Kanisa Katoliki linahitaji kubadili namna ya mahubiri yake na namna linavyoonekana.

      “Kanisa labadili mtindo wake!” likatangaza gazeti la Kifaransa Le Figaro. Kwa msherehekeo wa 12 wa Siku za Vijana Ulimwenguni katika Paris, kanisa lilitumia mashirika ambayo yana uzoefu wa kupanga maonyesho ya muziki wa roki yasimamie maonyesho haya. Kulikuwa na maonyesho zaidi ya 300 ya kutumbuiza vijana waliozuru kutoka zaidi ya nchi 100, na hasa makasisi wakashonewa mavazi ya kimtindo.

      Kwa kukosa kuwaelewa vijana wa leo na kuona uhitaji wa kubadilika, dini nyingi zinakuwa na imani zinazohusisha kila aina ya watu. Akidhihirisha sera hii, Michel Dubost, kasisi aliyepanga Siku za Vijana Ulimwenguni katika Paris, alisema hivi: “Bila shaka ningependa wote waliobatizwa wawe waaminifu kwa Kristo. Lakini hata ikiwa si waaminifu, wanakubalika kanisani.”

      Vijana Watafuta Majibu

      Likikazia kwamba kwa kweli vijana wanatafuta majibu, gazeti moja la habari lilifafanua hudhurio la vijana kwenye msherehekeo katika Paris kuwa “ombi la kutaka imani badala ya wonyesho wa imani.” Je, ombi hilo lilijibiwa na Kanisa Katoliki?

      Unapochunguza ndani badala ya nje au kuchunguza kile kilichoitwa na gazeti moja la habari la Kikatoliki kuwa “njozi za uongo” za misherehekeo mikubwa ya kidini, unapata nini? Gazeti la habari la Kifaransa Le Monde lilieleza kwamba kwa ndani kuna “ukosefu wa uradhi wa kweli.”

      Ingawa namna chakula kionekanavyo ni jambo la maana, chakula chapaswa kuwa chenye lishe. Maswali ya vijana kuhusu kusudi la maisha huhitaji majibu yenye kuimarisha kiroho. Vijana hawaridhishwi na majibu wanayopewa yenye kupendeza lakini yasiyokuwa na maana.

      Je, matukio ya kidini yasiyokuwa na maana yoyote yanawaathiri vijana wa leo kwa kudumu? Mwanasosholojia Mfaransa Danièle Hervieu-Léger alisema hivi: “Matukio haya yaliyopangwa vizuri ajabu hayawezi kutokeza athari za kijamii za kudumu.” Basi ni wapi vijana wawezapo kupata majibu yenye kuridhisha kwa maswali yao?

  • Vijana Hupendezwa na Dini Kadiri Gani?
    Amkeni!—1998 | Agosti 8
    • [Picha katika ukurasa wa 12]

      Msherehekeo wa kidini wavutia maelfu ya vijana katika Paris

      [Picha katika ukurasa wa 13]

      Siku za Vijana Ulimwenguni katika Paris—je, kweli ni kurudia kupenda dini?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki